Mbele ya waandishi wa habari na kingereza chake cha kuokota Pep Guardiola akasema, “Phil Foden is the greatest talent I have ever managed”. Hakuna aliyemuelewa Pep Guardiola, hata mimi sikumuelewa.
Subiri kwanza, huyu ndiyo mtu aliyempandisha Messi kutoka La Masia pale Barcelona, huyu mtu amemfundisha Andres Iniesta, huyu mtu anafanya kazi na David Silva na Kelvin De Bruyne. Anamaanisha kweli kuhusu Foden??
Labda kingereza kinampiga chenga, labda lugha ya malkia inamkataa, labda alitaka kuzungumza vingine lakini tulimuelewa tofauti kwasababu hii si lugha yake ya kwanza.
Lakini hapana Pep Guardiola hakuwa na masihara, alikuwa anamaanisha. Siku David Silva anatangaza kuondoka Pep Alirejea tena kusema, msiniulize namsajili nani kuziba nafasi ya Silva, pengo la Silva tumeshaliziba, yupo Phil Foden, ana kipaji kuliko David Silva.
Hakuna aliyemuelewa tena, tulijua tu ni Pep na zile stori zake za kumkataa Toni Kroos kwasababu anapenda sana kufunga kutokea mbali badala ya kupiga pasi za mwisho kwa washambuliaji. Hakuna aliyewahi kumuelewa Pep.
Siku zinaenda na muda haugandi, Foden kwenye kiungo cha Manchester City anasahaulisha kuwa David Silva ameondoka The Citizens na Kelvin de Bruyne yupo juu ya kitanda cha hospitali anapatiwa matibabu.
Phil Foden ana miaka 20, Pep alimzungumzia akiwa na miaka 17. Pep alitudanganya au kutuambia ukweli?? Tunaogopa kujibu kwasababu hakuna aliyewahi kumuelewa Pep.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Samira
Pep yupo sahihi kabisa
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri
Dorophina
Pep yupo sahihi kabisa
Magdalena
Kijana yupo vizuri
Sania
Yupo sahihi
Sadick
Foden anahitaji mentor kama Pep ili aendeleze kipaji chake. Vijana wengi hupoteza uwezo uwanjani kwa sababu ya mambo nje ya uwanja
Hopemwaikuka
Yuko vzur sana
Rahma
Yuko poa sana
Sarah
Yuko sahihi
Adelta
Inapendeza
warda
Kasena hivi anamkubali sana foden