Phil Jones Afanya Mazungumzo na Klabu ya Bordeaux

Mlinzi wa klabu ya Manchester United Phil Jones yupo kwenye mazungumzo na klabu ya Bordeaux ili aweze kujiunga nayo kwa mkopo hadi mwisho wa msimu.

Jones ambaye alikuwa nje ya kikosi cha wakubwa kwa muda mrefu, kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka miwili aliweza kurudi kwenye timu hiyo kwenye mchezo dhidi ya Wolves ambao Man Utd waliweza kushinda 1-0.

Phil Jones

Phil Jones kwa sasa anahitaji kurudisha makali yake na anaona akiendelea kubaki kwenye klabu ya Man Utd hataweza kupata nafasi tena, kutokana na ushindani uliopo kwenye nafasi ya ulinzi wa kati kutokana na uwepo Harry Maguire, Victor Lindelof, Raphael Varane na Eric Bailly.

Phil Jones alijiunga na klabu ya Man Utd mwaka 2011 kwa ada ya uhamisho wa £16.5milioni, baada ya kufanya mazungumzo na uongozi Jones amepewa ruhusa ya kutafuta klabu ya kwenda, klabu ya Bordeaux imeonesha nia ya kuhitaji huduma yake na mpaka habari inatoka bado wapo kwenye mazungumzo.


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe