Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba amejitokeza na kumtetea kocha wake Ole Gunnar Solskjaer kutoka kwenye kejeli za Mourinho kuhusu malezi.
Pogba anadai kuwa Mourinho ni mtu ambaye anapenda kupingana na wachezaji muda wote na huamua kuwatenga bila sababu yoyote, tofauti na kocha wake wa sasa Ole Solskjaer ambaye ana maelewano mazuri na wachezaji na hata kama ataweka benchi wachezaji fulani anatambua uwepo wao.
Paul anasema kwamba yeye na Mourinho walikuwa wanaelewana sana mpaka pale iliposhindikana. Na mpaka kesho hawezi kusema kilitokea nini kati yao. Mourinho amekuwa akihusishwa na tabia za kupenda kuwakomoa wachezaji ambao hawafuati matakwa yake.
“Ole ni wa tofauti sana na hawezi kupingana na wachezaji kama Mourinho… Ole anaweza asikuchague kwenye mechi lakini anatambua uwepo wako, tofauti na Mourinho. Na hiyo ndiyo tofauti yao kubwa” Aliandika Pogba kwenye post yake ya tweeter.
Maneno hayo yalikuja siku kadhaa baada ya kejeli za kurushiana maneno kati ya Ole na Mourinho ambayo yalitokana na kujiangusha kwa Son kwenye mechi kati ya Tottenham na Man United, ambapo Man united walishinda 3-1.
Mourinho alionekana kumkejeli Ole kutokana na kumsema sana Son ambaye alidai kufanyiwa faulo na Mc Tominay katika mechi hiyo, kitendo ambacho kilipelekea kufutwa kwa goli la Cavani.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.
Venerose
Paul yupo sahihi
Sarah
Poul yupo makini
Adelta
Mourinho inabidi ajiangaliye kwa sababu sio picha nzuri kwa wachezaji
dorophina
Pogba yupo sahihi ole ni kocha mzuri sana
warda
Binadam hatupo sawa