Aston Villa ndiyo inaongoza katika mbio za kumwania winga wa Paris Saint-Germain (PSG), Ibrahim Mbaye, mwenye umri wa miaka 18.

Ingawa Paris inataka kumbakiza mchezaji huyo baada ya kuonyesha kiwango kizuri, klabu hiyo haiwezi kumpa uhakika wa kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza.
Kipa kijana wa Paris, Renato Marin mwenye umri wa miaka 20, ambaye alisajiliwa kutoka AS Roma mwaka 2025, alicheza mechi tatu msimu uliopita.
Sasa ataichezea CD Nacional kwa mkopo katika msimu wa 2026/27 ili kupata uzoefu zaidi, kabla ya Paris kufanya tathmini ya maendeleo yake majira ya kiangazi mwaka ujao.
Kwa upande wa Lucas Chevalier, kipa huyo alipoteza kiwango chake, akapokonywa nafasi ya kwanza na Matvey Safonov na pia akakosa nafasi katika kikosi cha Ufaransa cha Taji la Dunia 2026.



