Barcelona wameripotiwa kukasirishwa na Paris Saint-Germain katika harakati zao juu ya mshambuliaji anayetaka kuondoka Barca Lionel Messi.
Mshindi huyo wa tuzo ya Ballon d’Or mara sita anapaswa kuwa mchezaji huru msimu wa joto na anaweza kufungua mazungumzo na vilabu vingine baada ya kufikia miezi sita ya mwisho ya mkataba wake ya Camp Nou.
Meneja wa PSG Mauricio Pochettino na mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Leonardo wamezungumza juu ya matarajio yao juu ya Messi kufanya biashara yake katika mji mkuu wa Ufaransa – maoni ambayo yanadaiwa kuwatibua Barcelona.
Taarifa zinasema, wababe hao wa Kikatalani wanahisi kuwa PSG wanajaribu kucheza michezo ya akili na Messi, ambayo wanahisi imevunja kanuni ya heshima kati ya vilabu hivyo viwili.
Ripoti hiyo pia inadai kwamba Barca wanaamini PSG wanajaribu kupata faida ya kisaikolojia kabla ya pambano lao la hatua 16 bora la Ligi ya Mabingwa, na mzunguko wa kwanza utafanyika mnamo Februari 16.
Hata hivyo, mshahara wa sasa wa Messi wa pauni 500k kwa wiki inaweza kudhaniwa kuwa ghali sana hata kwa PSG, wakati Manchester City wanahesabiwa kama kilabu kingine pekee kinachoweza kupata makubaliano.
Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.
Sylvester
Mesi aachane na PSG aje EPL kumenoga kwa wababe wa soka
Adelta
PSG wanataka kumsajili Messi
Magdalena
Psg hawana pesa za kumsajili Messi
Dorophina
Psg wanazingua awana mkwanja Messi inabidi atafute klabu yenye manufaa kwake
Sadick
PSG wanatupa ndoana kijanja,tusubiri kuona kama Messi atanasa. Utakuwa usajiri wa kushitua Ulimwengu
Shakila mrope
Habari njema
Angelina
Messi abaki tu barcelona
felister
Messi nae ata haelewekiii
Revina
Messi kwanza atajishusha sana kwa kiwango alichonacho sio wa kwenda PSG
Sarah
Messi nae hata hasomeki
Venerose
Messi anatakiwa aangalie wapi panamfaha
Rahmal
Messi nae anangaika atulie sehemu moja
Ernest Kimeru
Messi ataanza kusumbua tena vichwa vya habari
Caroline
Messi anawasumbua kweli
Lydia Emmanuel Magoti
Messi akili nyingi
Emmanuel dalaya
Aondoke tu ili apate changamoto zngne
Sania
Messi anapata misukosuko mingi sana
Tatu
Mess yupo vizuri
Issa
Man city ndio patamfaa
Hopemwaikuka
Sawa tu
Amani Maeda
Huyu jamaa ufundi wake unahitajika
warda
Barca wanampenda sana Messi