PSG imekubali kumuuza Gonçalo Ramos kwenda AC Milan kwa ada ya rekodi katika historia ya klabu hiyo ya Italia.

Mshambuliaji huyo tayari amefanyiwa vipimo vya afya nchini Marekani (Florida) na anaondoka PSG baada ya kucheza mechi 131 na kufunga mabao 45, huku pia akicheza katika fainali ya UEFA Champions League.
Inadaiwa kuwa kocha Ruben Amorim alikuwa na mchango mkubwa katika kushinikiza usajili huo.
Wakati huohuo, PSG imethibitisha kuwa itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mallorca tarehe 5 Agosti kwenye Uwanja wa Son Moix. Mchezo huo unatarajiwa kuwa sehemu ya mwisho ya maandalizi ya msimu mpya kabla ya kuivaa Aston Villa katika UEFA Super Cup tarehe 12 Agosti, kisha kucheza dhidi ya Lens kwenye Trophée des Champions tarehe 16 Agosti.



