SAED Ramovic, Kocha Mkuu wa Yanga ameweka wazi kuwa ni lazima wachezaji waendelee kupambana kwenye mech izote ili kupata matokeo mazuri ndani ya uwanja.
Yanga kwenye mchezo uliopita wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Namungo uliochezwa Uwanja wa Majaliwa uliwakosa wachezaji watatu ambao hawakuwa fiti ni Ladack Boka, Khalid Aucho na Clement Mzize.Mwisho mchezo huo wa pili kwa mrithi mikoba ya Miguel Gamondi ubao ulisoma Namungo 0-2 Yanga kwa mabao ya Kennedy Musonda na Pacome.