Hali ya Marcus Rashford na Manchester United imeingia tena kwenye sintofahamu. Baada ya mkopo wenye mafanikio Barcelona msimu uliopita, United walitarajia sana kwamba Barça wangechukua chaguo lao la kumnunua kwa £26m (€35m). Lakini klabu ya Catalonia iligeukia njia nyingine ya kumsajili Anthony Gordon kutoka Newcastle kwa £69m, na Rashford akabaki njia panda.

Kwa macho ya mashabiki, ujio wa kocha mpya Michael Carrick, aliyewahi kuwa mchezaji mwenzake, ungeweza kumrahisishia kurudi kikosini. Lakini hali si rahisi. United wanaweza kumtoa tena kwa mkopo, au kumuuza moja kwa moja, na uamuzi huenda ukachelewa hadi mwisho wa dirisha la usajili.
Rashford alitarajiwa kuonyesha kiwango kikubwa na England kwenye Kombe la Dunia 2026, lakini nafasi yake ilichukuliwa na Gordon. Alimaliza mashindano na bao moja na asisti moja pekee, akipoteza nafasi ya kuongeza thamani yake sokoni.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Chaguo za Usajili Zimefifia kwa Rashford kwani Barcelona hawakutumia kipengele cha kumnunua moja kwa moja, na United hawataki kurudia mazungumzo, exit clause ya £40m ilimalizika Julai, ikimaanisha ada mpya lazima ijadiliwe.

Rashford amekataa ofa kutoka Fenerbahce na Galatasaray, akishikilia ndoto ya kujiunga na klabu kubwa ya Champions League. Na United walikuwa wakimfikiria Crysencio Summerville wa West Ham, lakini sasa anaelekea Al-Hilal kwa £60m. Sasa anaendelea kusubiri ofa kutoka klabu kubwa barani Ulaya, huku muda ukisogea na dirisha la usajili likikaribia kufungwa.


