Real Madrid inaweza kuwa inajiandaa kwa moja ya operesheni kubwa zaidi za usajili katika majira haya ya joto huku rais wa klabu, Florentino Perez, akichunguza uwezekano wa kumsajili winga wa Bayern Munich, Michael Olise, katika dili ambalo linaweza kuhusisha kiasi kikubwa cha fedha pamoja na kuondoka kwa mmoja wa viungo muhimu wa kikosi cha kwanza.




