Richarlison De Andrade amezaliwa tarehe 10 mwezi mei mwaka 1997, Richarlison ni chotara wa ki Brazili na Ureno na ni mchezaji wa timu ya taifa ya Brazili anaekipiga katika timu ya Everton inayoshiriki katika ligi kuu ya Uingereza.
Kinda huyo alianza safari yake ya soka katika timu ya America Mineiro mwaka 2015, na kupata nafasi ya kucheza kikosi B cha timu ya Campeonato Brasileiro kwa msimu mmoja tu kabla kabla ya kwenda Fluminese. Na kucheza mechi 67 na kufunga nagoli 19 ndani ya miaka miwili ya utumishi wake kilabuni hapo. Baada ya mafanikio katika vilabu vya nyumbani Richarlison akajiunga na Watford na mwaka mmoja badae akajiunga na Everton.
Utumishi wake Everton umefanya amekua mchezaji muhimu saana na umuhimu wake mkubwa ni katika safu ya ushambuliaji, Kwa msimu wa 2019/20 pekee ana rekodi ya kumiliki mpira mara nyingi ndani ya 18 ya timu pinzani, wakati 10 kati ya magoli yake yote yakitokana na mshambuliaji mwenzie Calvet Lewin.
Mvuto wa Richarlison hauishii kwenye uwezo wa kushambulia yeye kama yeye, Ikumbukwe kua Richarlison anarekodi pia ya kua msababishaji wa magoli ya washambuliaji wenzie.
Lakini licha ya mchango wake kama mshambuliaji, Mbrazili huyoamezuia mara nyingi Zaidi kuliko mshambuliaji mwingine yeyote kwenye Ligi kuu ya Uingereza, Amekaba mara 20 zaidi ya mshambuliaji yeyote kwenye ligi kuu ya Uingeleza.
Povel
Richardson mwamba sana