Roma Wanahusishwa na Allegri Baada ya Kutimua Kocha Wao

Kocha wa zamani wa Juventus, Massimiliano Allegri alikuwa  kwenye Uwanja wa Stadio Meazza mjini San Siro usiku wa jana  kutazama mechi kubwa ya Serie A kati ya Inter na Napoli huku akihusishwa na AS Roma.

Roma Wanahusishwa na Allegri Baada ya Kutimua Kocha Wao
 

Aliyekuwa kocha wa Juventus na Milan Allegri alikuwa San Siro kutazama mechi ya nyumbani ya Inter dhidi ya viongozi wa ligi Napoli usiku wa jana.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Bianconeri alimfukuza kazi mtaalamu huyo wa Italia mwezi Mei na kumaliza msimu akiwa na Paolo Montero kabla ya kumwajiri Thiago Motta.

Allegri ni miongoni mwa wagombea kuchukua nafasi ya Ivan Juric huko Roma, kwani mtaalamu huyo wa Croatia ametimuliwa baada ya mechi 12 pekee.

Roma Wanahusishwa na Allegri Baada ya Kutimua Kocha Wao
 

AS Roma mpaka sasa kwenye ligi wamecheza mechi 12 wakishinda mechi 3 pekee, sare 4 na kupoteza mechi 5 hadi sasa huku wakishikilia nafasi ya 12 na pointi zao 13 hadi sasa.

Mechi inayofauta baada ya mapumziko ya Kimataifa, watakipiga dhidi ya Napoli ugenini, ambapo Naples ndio wanaongoza ligi wakiwa wamewazidi kwa tofauti ya pointi 13.

Acha ujumbe