Ronald Koeman amekiri kwamba “hana imani” Lionel Messi atasalia Barcelona zaidi ya msimu huu.
Mshindi huyo wa tuzo ya Ballon d’Or mara sita ametumia taaluma yake yote ya soka huko Camp Nou, akichezea zaidi ya michezo 750 kwa miamba hao wa La Liga.
Leo alishindwa jaribio lake la kuondoka klabuni hapo msimu uliopita wa kiangazi, lakini anamaliza mkataba katika muda wa miezi minne na anaweza kuanza mazungumzo na vilabu vya kigeni kuhusu uhamisho bure kama mchezaji huru.
Barca alikuwa na matumaini ya kumshawishi Messi akubali masharti mapya, ingawa Koeman bado hana uhakika kama mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina atabaki Catalonia.
“Sina imani na hilo,” Koeman aliiambia The Athletic alipoulizwa ikiwa anafikiria Messi atasalia klabuni hapo.
“Nina matumaini, ndio, kwa sababu yeye bado ni mchezaji mzuri na bado anashinda mechi kwetu, kwa timu.
“Ninafurahiya kuwa kocha wake. Ukiangalia sifa zake na uwezo wake kila siku kwenye mazoezi, ni jambo la kufurahisha. Kwa kweli, alikuja akiwa mtoto mdogo huko Barcelona. Na bado sioni Leo Messi akiwa kwenye jezi nyingine zaidi ya jezi Barca. ”
Paris Saint-Germain na Manchester City wanachukuliwa kama mahali pekee Leo anaweza kwenda ikiwa ataondoka Barcelona msimu wa joto.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.
Caroline
Uyo Messi aende Barcelona..
Caroline
Uyo Messi aondoke tu Barcelona..
Magdalena
Messi kashachoka kukaa sehemu moja
Dorophina
Barcelona inabidi wakubali tu kuachana na Messi maisha yaendelee
Venerose
Messi kazi popote
Rahma
Kambi popote messi
Hopemwaikuka
Ila Messi unajiweza siku zote hzo
Sarah
Maisha popote messi
Amiri Kayera
Mess ataondk tu
Mwanahamisi
Kambi popote
Sania
Messi akiondoka Barcelona ataacha pengo kubwa
Lydia Emmanuel Magoti
Afanye mamuzi
warda
Kama huna imani nae si muache aende