Waziri wa michezo wa Italia, Vincenzo Spadafora, amesema kuwa uchunguzi umeanzishwa juu ya Cristiano Ronaldo.
Nyota huyo wa Juventus alikwea pipa na kurejea nchini Italia ili hali aligundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya korona wakati akiwa kwenye majukumu ya kuitumikia timu yake ya taifa, Ureno takribani majuma mawili yaliyopita.
Ronaldo amekuwa akijifungia nyumbani kwake mjini Turin tangu agundulike ana Covid-19 hivyo kupelekea kuukosa mtanange dhidi ya Crotone na ule dhidi ya Dynamo Kiev siku ya Jumanne.
Spadafora alishika vichwa vya habari baada ya kukemea kitendo cha Ronaldo kurejea nchini Italia, akidai kuwa hakuheshimu taratibu zilizowekwa na mamlaka za afya.
Ronaldo kusikia hivyo akajibu kwa kupitia ‘Instagram live video’ akiwa karantini akidai kuwa taarifa hizo zinazomdai kakiuka taratibu za mamlaka ya afya ni za uongo.
“Ninaheshimu taratibu na kanuni zilizowekwa, hamna nilipokiuka, kama ilivyosemekana; wote huo ni uongo,”
”Nilirejea kutoka Ureno mara baada ya timu yangu na mimi kujiridhisha kuwa taratibu zote za msingi zimefuatwa. Nimerejea Italia kwa ‘Air ambulance🛫’ na sijakutana na mtu yeyote, hata hapa Turin”.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
warda
Jamani wanataka kumchafua tu ,daa sio poa
Dorophina
Dhuu sasa itakuwaje kama mwenyewe Ronaldo anakanusha sio kweli
Hopemwaikuka
Kwan we wazir ulitakaje sasa mtu pesa ipo acha ajiuguze mwenyewe anavyoweza
Adelta
Hapo itakuaje??
Mwajumah
Daah sio poa kabisa hii wanataka kumualibia tu Ronaldo
Mwanahamisi
Daah sio poa
Ernest
Hizi ni changamo za Corona
Elika
Corona sio poa
Angelina
Corona inaleta kuzaazaa
aisha
Duuuh ugonjwa huu
Fatuma kasomo
Sio poa
Neema
Coronaa inaletaa majangaa zaidi
Janeflora malisa
Dah
Povel
Sheria ifuate mkondo wake hapo
Issa
Cr afate mashart
Sabrina
Dah CR7 tulia basi mambo yakae sawa upone
Saupha mohamed
Afate masharati
Latifa juma mohamed
Corona inaleta Mambo meusi.
David Pere
Ronaldo amekuwa akijifungia nyumbani kwake mjini Turin tangu agundulike ana Covid-19 hivyo kupelekea kuukosa mtanange dhidi ya Crotone na ule dhidi ya Dynamo Kiev siku ya Jumanne.
Zahara Omary
Daah sio poa
Sauda
Corona imeleta majanga
zeiyana
ni vizuri vigezo na masharti kuzingatiwa usalama ndio kitu kizuri maana huu ugonjwa ni hatari sana
Lydia Emmanuel Magoti
Duu changamoto za gonjwa la Corona hizi