Cristiano Ronaldo anasisitiza kuwa “hajawahi kumuona Lionel Messi kama mpinzani” baada ya Juventus kumalizana na kibarua kizito cha kuichapa Barcelona 3-0 huko Camp Nou.
Juventus walilazimika kushinda magoli zaidi ya mawili ili kufuta ushindi wa Barcelona, ambao waliupata pale Turin wa bao 2-0.
Magoli mawili ya penati yaliyowekwa wavuni na Cristiano na moja zaidi lililowekwa na Weston McKennie, wakati Gigi Buffon akifanya kazi nzuri kuzuia mikwaju yote saba ya Messi golini iliwaacha Barcelona wakimaliza mechi chali, tumbo likiyatazama mawingu.

CR7 ambaye anabainisha kuwa kibarua dhidi ya Barca hakikuwa cha kitoto, aliweka wazi kuwa waliamini wanaweza kupindua Meza mapema katiika dakika 20 baada ya kujihakikishia magoli 2-0, katika safari ya kulisaka goli la 3.
Barcelona hawakufurahishwa na adhabu ya kwanza, iliyotolewa wakati Ronald Araujo alipoingia kwenye mvutano na Ronaldo.
Ronaldo alipotakiwa kuzungumzia uhusiano wake na Messi, na kama huwa anamchukulia kama mshindani. Alisema kuwa wamekuwa pamoja katika sherehe nyingi takribani miaka 12 hadi 13, na hauwahi kumchukulia kama mpinzani wake.
“Tumekuwa kwenye sherehe za tuzo kwa miaka 12-13 sasa na sikuwahi kumuona kama mpinzani, hiyo yote imechochewa na vyombo vya habari. Siku zote tulielewana vizuri na ukimuuliza Leo, atakuambia hivi hivi.” Ronaldo
MALIZA MWAKA KIBINGWA KWA KUJISHINDIA SHEA YAKO KWENYE SHILINGI 140,000,000TSH!!
Kipindi hiki cha sikukuu kinamalizika kwa namna ya kipekee. Shilingi 140,000,000 kushindaniwa katika michezo ya Evolution kwenye Kasino Mubashara ya Meridanbet. Ingia mchezoni na ujiwekee nafasi ya kushinda shea yako!!!
Tatu
Wakikutana nje ni washikaji ila Wakikutana uwanjani ni mpizani wake
warda
Walijitahidi sana
Povel
Duh hizi ni kejeri baada ya kupata matokeo juzi
Ester jackson
Safii hii ni zuri sana mana water ni wachezaji wanatakiwa kucheza kwenye nafasi zao lakini wanapokuwa faraga basi itawalazimu wawe marafiki
Caroline
Safi sana.nimependa mtazamo wake
Farida ahmad
Ni mtazamo wake