Klabu ya RS Berkane ya Morocco imetwaa taji la Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuifunga Orlando Pirates ya Afrika Kusini kwa penati 5-4 katika fainali iliyochezwa Uwanja wa Godswill Jijini Uyo, Nigeria.
Dakika 90 zilikamilika timu hizo zikiwa sare tasa, Berkane walikuwa wa kwanza kuandika goli dakika ya 97 kwa mkwaju wa penati kabla ya Orlando kusawazisha dakika ya 117 katik adakika 30 za nyongeza.

Hadi dakika 120 za muda wa maongezi zinakamilika kabu hizo zilimaliza kwa bao 1-1. Berkane walitwaa ubingwa kwa penati 5-4 baada ya Thembinkosi Lorch wa Pirates kukosa penati yake.
Kabla ya fainali Orlando Pirates iliongoza Kundi B, ikaiondoa Simba Robo Fainali na kuifunga Al Ahli Tripoli mabao 2-1 katika Nusu Fainali.
RS Berkane iliongoza Kundi D, ikaiondoa Al Masry kwa faida ya bao la ugenini katika Robo Fainali na ikaifunga TP Mazembe 4-2 katika Nusu Fainali.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.



