Saidi Ntibazonkiza na Miguu ya Ajabu

Wakati Waholanzi kwenye Jiji la Rotterdam ndani ya dimba la Goffer wakishangilia kwa nguvu zote ili timu yao Feyenoord isawazishe dhidi ya NEC, ilikuwa bahati mbaya sana kwao hawakujua dakika chache zijazo nini kinakuja

Iliwekwa pass Moja ndefu sana kutoka kwa Golikipa wa NEC, ikaguswa na Midfielder mmoja kisha akaisukuma mali kwenye miguu ya Sniper mmoja wa hatari, katikati ya msitu wa mabeki

Akaicontrol ile mali, akaigusa touch ya kwanza kasi, akaigusa touch ya pili kwa akili, anatembea katikati ya mabeki wawili, akawatisha kulia na wakajaa kushoto, akamsalimia Golikipa kwenye nyavu za juu

Uwanja ukatulia kwa sekunde kadhaa, Saido Ntibazonkiza tayari anawakumbusha thamani ya miguu yake ya Kirundi, kila mtu alikubali, hii ilikuwa 2008 ligi kuu Uholanzi, alichofanya miaka 12 bado alikifanya jana kwa Kaseke

Uholanzi ilimuhusudu sana, lakini Mungu kaleta fumbo kubwa sana kwa watu wenye vipaji, kuna vitu katuficha kawapa maarifa, ujasiri na roho za kitajiri ila kuna namna kawafumba sehemu, fumbo la imaan

Saido nilimuona tena Ufaransa mechi kati ya Caen na Rennais, game tayari ngumu na dakika zinayoyoma na ushindi ni muhimu kwa Caen, kumbuka ni Ligi Kuu Ufaransa, Kocha anaagiza mipira yote ifikishwe miguuni mwake

Kaunta ya kwanza inafika kwa winga wa Caen, kisha ya pili inafika kwa straika wao, inawekwa kipa anaicheza, inawekwa ya pili beki anakataa, touch ya tatu inatua kwa Saido

Licha ya kuwa kwenye presha kubwa na nje kidogo ya 18, anaivuta mali, anachungulia wapi pakuweka na kumsabahi Golikipa, ngoma inaisha 1-0, Saido anaokoa siku kwa Caen

Hakuna jipya chini ya jua, Saido anaendeleza pale alipoishia, yaliyotokea yote ni fumbo la imaani, tuendelee kufaidi kipaji chake kinachoelekea mwishoni, Saido tulisafiri nyuma ya muda na sasa tupo mbele ya muda.


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???

SOMA ZAIDI

12 Komentara

    Anakipaji kizuri san tuenderee na kufaidi na kipaji chake

    Jibu

    Mmh wape salaam saiid watamwez fund

    Jibu

    Jamaa yupo vizur

    Jibu

    Jamaa namuelewa

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Said ntibazonkiza ni mwenye kipaji Cha kuzaliwa

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Amazing

    Jibu

    Ntibazonkiza anajua sana

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Yuko Safi tu

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

Acha ujumbe