Klabu ya Aston Villa imemteua Craig Shakespeare kuwa kocha msaidizi wa timu hiyo akichukua nafasi ya John Terry.
John Terry alikuwa msaidizi wa Dean Smith katika kukinoa kikosi cha Aston Villa kilichopambana kubaki Ligi Kuu Uingereza- EPL. Aston Villa ambayo ilipanda daraja msimu uliopita, walikuwa na wakati mgumu kupambana kusalia kunako EPL msimu ujao.
Terry amekuwa akipewa lawama za mara kwa mara kwa kushindwa kutumia uzoefu wake kama beki hodari kuboresha safu ya ulinzi ya Aston Villa. Pamoja na changamoto zote, Terry kwa kushirikiana na Dean Smith walifanikiwa kuibakiza Villa kwenye Ligi Kuu Uingereza – EPL baada ya Watford kupoteza mchezo wao wa mwisho dhidi ya Arsenal.
Shakespeare anauzoefu mkubwa na EPL akiwa amewahi kufanya kazi na Claudio Ranieri kukinoa kikosi cha Leicester City. Katika wakati wake na Leicester City, walifanikiwa kubeba kombe la Ligi Kuu Uingereza – EPL mwaka 2015/16.
Craig Shakespeare Akitoa maelekezo kwa wachezaji wa Leicester City.
Taarifa rasmi kutoka katika ukurasa wa Aston Villa zinasema ” Nilikuwa ninahitaji kuongeza mkufunzi mahiri wa Ligi Kuu Uingereza – EPL katika benchi langu la ufundi, Craig anakila sifa katika hilo.”
” [Shakespeare] anauzoefu mkubwa, atatuongezea viwango vingine katika timu yetu. Nimemfaham Craig kwa muda mrefu, tangu kipindi tunacheza Walsall. Ninatarajia mazuri katika kufanya nae kazi” Alisema kocha mkuu wa Aston Villa – Dean Smith.
Craig amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi katika Ligi Kuu Uingereza – EPL na ligi daraja la kwanza – Championship.
Akiwa na miaka 56 [Craig Shakespeare], amewahi kuwa kocha msaidizi na pia, amewahi kuwa kocha mkuu. Kwa ujumla amekuwa kwenye benchi la ufundi kwa takribani miaka 20 akishiriki michezo 500.
Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.
Shafii
Terry licha ya kua mzoefu tu katika safu ya ulinzi kwa upande mwengine ilipaswa avumiliwe kwani bado ni kinda Sana katika sector ya ukocha na anasafari ndefu ya kuja kua kocha mzoefu.
Mwajumah
Namkubali sana Terry ni kocha mzuri sana# Meridianbettz
Ernest
Nadhani Craig Shakespeare atakuja na mbinu zake mpya zitakazo isaidia Aston Villa
Adelta
Asante kwa makala nzuri
#meridianbettz
Zeiyana
Clabu yingi zimekua zinaitaji sana makocha vijana craing Shakespeare ni kocha mwenye mbinu yingi tunategemee matokea mazuri kutoka kwake
Mwanahamisi
Terry ni kocha mzuri
Khadija
Terry kocha anayejua nn anachokifanya#meridianbettz
Dorophina
Angetulia kwanza asinge ingia kwenye ukocha maana bado anakibarua kizito cha kujiweka kwanza yy vizuri
Zeiyana
Shakespeare ni kocha mwenye mbinu za haina yake
Caroline
Shakespeare ataleta mafanikio makubwa kwa Astonvilla
Fatina mfingi
Terry Ni kocha mnzur
Nasra
Kocha mzuri sana
Lydia Emmanuel Magoti
Safii Sana nikocha anaejierewa
aisha
Terry yuko vizuri sana
Sadick
Unaweza kuwa mwanafunzi mzuri lakini usiwe mwalimu mzuri. Terry bado hajakomaa kuwa kocha mwenye mafanikio,anahitaji muda. Aston Villa imeona mapungufu na kuamua kubadili mwelekeo#meridianbettz
Janeflora malisa
Good
Tatu
Terry ni kocha nzuri nzuri
magdalena
terry kuwA KOCHA AFANYE SANA JUHUDI
Devotha
Tusubiri kuona ubora wake kwenye msimu ujao ndo tutajua kama ni kocha bora au la!!!
felister
shakespeare ana uzoefu mkubwa
Furahav
Haya nenda kakibadirishe kikosi cha Aston villa.
Hope mwaikuka
🙊
farida ahmadi
Asante kwa taarifa
Saupha mohamed
Good news
Amiri Kayera
Habar nzur
Johnmary joel
Habari nzuri# meridianbett
Latifa juma mohamed
Terry kocha safi
David Pere
Ndio kazi yeki Kama kocha anayetengeneza CV yake
Genia Sikaluzwe
Habari nzuri
Ester jackson
Bado sana kwa kocha mana katika uchezaji wake alikuwa vizuri ila bado hajastahili kuwa kocha sio kitu cha wepesi
Samiah
Gud
Sabrina
Karibu Aston villa
Omary lukumbi
Terry angeenda tuu kua mchambuz kuliko hyo kali anayo ifanya au basi akaunge nguvu na frank lampard kwenye kikos cha Chelsea kama marejendari wawili waliochezea club moja
warda
Terry anatiaga huruma sana