Shakespeare Achukua Nafasi ya Terry

Klabu ya Aston Villa imemteua Craig Shakespeare kuwa kocha msaidizi wa timu hiyo akichukua nafasi ya John Terry.

John Terry alikuwa msaidizi wa Dean Smith katika kukinoa kikosi cha Aston Villa kilichopambana kubaki Ligi Kuu Uingereza- EPL. Aston Villa ambayo ilipanda daraja msimu uliopita, walikuwa na wakati mgumu kupambana kusalia kunako EPL msimu ujao.

Dean Smith na John Terry
Dean Smith na John Terry

Terry amekuwa akipewa lawama za mara kwa mara kwa kushindwa kutumia uzoefu wake kama beki hodari kuboresha safu ya ulinzi ya Aston Villa. Pamoja na changamoto zote, Terry kwa kushirikiana na Dean Smith walifanikiwa kuibakiza Villa kwenye Ligi Kuu Uingereza – EPL baada ya Watford kupoteza mchezo wao wa mwisho dhidi ya Arsenal.

Shakespeare anauzoefu mkubwa na EPL akiwa amewahi kufanya kazi na Claudio Ranieri kukinoa kikosi cha Leicester City. Katika wakati wake na Leicester City, walifanikiwa kubeba kombe la Ligi Kuu Uingereza – EPL mwaka 2015/16.

Shakespeare
Shakespeare akiwa na wachezaji wa Leicester City

Craig Shakespeare Akitoa maelekezo kwa wachezaji wa Leicester City.

Taarifa rasmi kutoka katika ukurasa wa Aston Villa zinasema ” Nilikuwa ninahitaji kuongeza mkufunzi mahiri wa Ligi Kuu Uingereza – EPL katika benchi langu la ufundi, Craig anakila sifa katika hilo.”

” [Shakespeare] anauzoefu mkubwa, atatuongezea viwango vingine katika timu yetu. Nimemfaham Craig kwa muda mrefu, tangu kipindi tunacheza Walsall. Ninatarajia mazuri katika kufanya nae kazi” Alisema kocha mkuu wa Aston VillaDean Smith.

Craig amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi katika Ligi Kuu Uingereza – EPL na ligi daraja la kwanza – Championship.

Akiwa na miaka 56 [Craig Shakespeare], amewahi kuwa kocha msaidizi na pia, amewahi kuwa kocha mkuu. Kwa ujumla amekuwa kwenye benchi la ufundi kwa takribani miaka 20 akishiriki michezo 500.


Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.

Ingia Mchezoni

34 Komentara

    Terry licha ya kua mzoefu tu katika safu ya ulinzi kwa upande mwengine ilipaswa avumiliwe kwani bado ni kinda Sana katika sector ya ukocha na anasafari ndefu ya kuja kua kocha mzoefu.

    Jibu

    Namkubali sana Terry ni kocha mzuri sana# Meridianbettz

    Jibu

    Nadhani Craig Shakespeare atakuja na mbinu zake mpya zitakazo isaidia Aston Villa

    Jibu

    Asante kwa makala nzuri
    #meridianbettz

    Jibu

    Clabu yingi zimekua zinaitaji sana makocha vijana craing Shakespeare ni kocha mwenye mbinu yingi tunategemee matokea mazuri kutoka kwake

    Jibu

    Terry ni kocha mzuri

    Jibu

    Terry kocha anayejua nn anachokifanya#meridianbettz

    Jibu

    Angetulia kwanza asinge ingia kwenye ukocha maana bado anakibarua kizito cha kujiweka kwanza yy vizuri

    Jibu

    Shakespeare ni kocha mwenye mbinu za haina yake

    Jibu

    Shakespeare ataleta mafanikio makubwa kwa Astonvilla

    Jibu

    Terry Ni kocha mnzur

    Jibu

    Kocha mzuri sana

    Jibu

    Safii Sana nikocha anaejierewa

    Jibu

    Terry yuko vizuri sana

    Jibu

    Unaweza kuwa mwanafunzi mzuri lakini usiwe mwalimu mzuri. Terry bado hajakomaa kuwa kocha mwenye mafanikio,anahitaji muda. Aston Villa imeona mapungufu na kuamua kubadili mwelekeo#meridianbettz

    Jibu

    Good

    Jibu

    Terry ni kocha nzuri nzuri

    Jibu

    terry kuwA KOCHA AFANYE SANA JUHUDI

    Jibu

    Tusubiri kuona ubora wake kwenye msimu ujao ndo tutajua kama ni kocha bora au la!!!

    Jibu

    shakespeare ana uzoefu mkubwa

    Jibu

    Haya nenda kakibadirishe kikosi cha Aston villa.

    Jibu

    🙊

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Habar nzur

    Jibu

    Habari nzuri# meridianbett

    Jibu

    Terry kocha safi

    Jibu

    Ndio kazi yeki Kama kocha anayetengeneza CV yake

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Bado sana kwa kocha mana katika uchezaji wake alikuwa vizuri ila bado hajastahili kuwa kocha sio kitu cha wepesi

    Jibu

    Gud

    Jibu

    Karibu Aston villa

    Jibu

    Terry angeenda tuu kua mchambuz kuliko hyo kali anayo ifanya au basi akaunge nguvu na frank lampard kwenye kikos cha Chelsea kama marejendari wawili waliochezea club moja

    Jibu

    Terry anatiaga huruma sana

    Jibu

Acha ujumbe