Cecrick Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa licha ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba kupelekwa mbele wanaamini kwamba wakikutana ndani ya uwanja lazima washinde.
Awali ratiba ilikuwa inaeleza kuwa mchezo huo wa watani wa jadi ulitarajiwa kuchezwa Februari 20, Uwanja wa Mkapa ila kwa sasa utachezwa Mei 8.
Kaze alisema kuwa hawana mamlaka ya kuzungumzia kuhusu kubadilishwa kwa ratiba ya mchezo ila wanachojua wao ni kwamba lazima watakutana ndani ya uwanja.
“Kubadilishwa kwa ratiba hiyo kwetu sio tatizo, kwa kuwa mamlaka imesema iwe hivyo sisi tunajipanga kwa ajili ya mechi zetu zijazo ambapo kwa sasa tupo kwenye maandalizi ya mchezo dhidi ya Mbeya City.
“Kwa kuwa tutakutana nao Mei 8 hiyo basi tunajipanga kuona kwamba tukikutana nao uwanjani tunashinda. Kwetu tunatazama mechi zote ni ngumu na ushindani ni mkubwa hivyo hatuna mashaka lazima tufanye vizuri,” alisema.
Mchezo wa raundi ya kwanza walipokutana uwanjani, Yanga ikiwa mwenyeji ngoma ilikamilika kwa sare ya kufungana bao 1-1, Uwanja wa Mkapa.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Magdalena
Maneno mengi hatutaki ngoja tuone
Rahma
Izo ni mbwembwe tu ngoja tuone itakuwaje
Angelina
Sisi mashabiki tunasubiri kwa hamu hiyo mei8
Dorophina
Maneno yasiwe mengi sana ni vitendo siku hiyo
Hopemwaikuka
Mmh
Sarah
Duuh
Ernest Kimeru
Ngoja tuone
Lydia Emmanuel Magoti
Ataanzaje kufa kwamfano wazee wakazi
Caroline
Paka FC hawana jipyaa
Sadick
Mechi ya Yanga na Simba haijawahi kuwa rahisi hata kama timu mojawapo haina kikosi mahiri
Sania
Simba sio timu ya kuibeza
warda
Asije kufa yeye tu