Tetesi za usajili dirisha hili dogo zinaendelea kupamba moto ambapo baadhi ya vilabu vinaendelea kufanya usajili ikiwemo Simba SC ambapo wao wamemsajili Nickson Kibabage kutoka Sindiga Black Stars.

Kibabage ambaye ni beki wa kushoto, amepewa mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba huku wakiwa na matumaini ya mchezaji huyo kufanya vyema na kuisaidia timu hiyo.
Mchezaji huyo amekuwa akionesha kiwango kizuri akiwa na Singida Big Stars, anatarajiwa kuongeza ushindani na uimara katika safu ya ulinzi ya Simba.
Ikumbukwe kuwa mchezaji huyo pia amewahi kukipiga mitaa ya Twiga na Jangwani yaani Yanga ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi hadi sasa lakini pia wakiwa na kiwango kizuri msimu huu.
Simba mpaka sasa kwenye mechi walizocheza wameshapoteza mechi moja na kutoa sare moja hapo juzi dhidi ya Mtibwa Sugar kutoka kule Morogoro huku matumaini ya wao kutwaa ubingwa wa NBC yakiaanza kufifia na mashabiki wa klabu hiyo wakiwa hawana imani na timu yao kutokana na matokeo ambayo wanayapata.


