Sergio Ramos na Real Madrid bado hawajakamilisha mazungmzo juu ya mkataba mpya wa nahodha huyu wa Los Blancos, lakini wakala wake anasisitiza hakuna sababu ya mtu yeyote kuwa na wasiwasi.
Ramos alijiunga na Madrid mnamo 2005 kutoka Sevilla na ameendelea kuwa muhimu sana kwa kilabu, amecheza karibu mechi 650 na kushinda tuzo nyingi.
Sasa akiwa na miaka 34, Mhispania huyu ni kama ana ukaribia usiku katika majukumu yake ya soka, lakini akiwa ameichezea Madrid mechi 25 kati ya 27 kwenye LaLiga kabla ya coronavirus, bado anaonekana kuwa mchezaji muhimu kwa Zinedine Zidane.
Mkataba wa Ramos unamalizika baada ya mwaka mmoja, na kuna maoni kuwa hatma yake ya muda mrefu pengine inaweza kuwa rehani ikiwa Madrid wataamua kutokuongeza mkataba wao.
Lakini wakala wa Ramos, ambaye ni kaka yake Rene, anaamini pande zote mbili zinataka nyota huyu astaafu soka akiwa Santiago Bernabeu.
“Soka linazunguka sana lakini kuna nia nzuri kwa pande zote mbili,” wakala huyo aliiambia Radio Marca.
“Natumaini atastaafu kwenye Real Madrid, ni ndoto yake na ninaelewa kuwa itakuwa nia ya kilabu pia.”
“Mpaka leo, hatujazungumza juu ya kitu chochote lakini hakuna haja ya kushtushwa. Wakati klabu itakapofikiria, tutaanza kuongea.”
Kwa maana hii, Sergio Ramos analazimika kusubiri maamuzi ya klabu ikiwa wataamua kumuongezea mkataba au lah! lakini matarajio makubwa ni kuwa atapata mkataba mpya.
mwakalosi
Madrid hawako tayari kumpoteza ramos japo ana umri mkubwa lakini ni mtu muhimu sana pale bernabeu
David Pere
Kama vipi astafuu tu aendelee kuweka heshima
Gabriel
Hatima ya mwisho ni kumsikiliza wakala wake yeye ndo ambaye anaeyemtafutia mchongo Kama mpaka anaongea na radio marca hivyo Kuna habari huenda akabaki kumalizia msimu wake akiwa wote akiwa Madrid
Furahav
Hatoki jeshi.
Shafii
Ramos Bado Sana real Madrid
Aziza mushi
Madrid wanamkubali sna Ramos japo anaumri mkubwa lakini bado yupo vizuri.
Evaluziga
Kama vip astaafu aendelee kuweka heshima
Salma
Wampe tu mkataba mpya bado yupo vizuri
Genia Sikaluzwe
Ramos Bado yuko vizuri wampe tu mkataba
Mwanaidi
Yupo vizuri sanaa
Hamidu
Ramos yupo vizuri! Me naona akatafute changamoto nyingine#meridianbettz
Tahiya
Ramos bdo yuko vizur aende Juve kwa wahenga wenzie
Antony Luseno
Ntafurahi endapo atabaki kuwepo Real Madrid maan ukitaja Madrid lazima umtaje Ramos
Leonard
Ramos bora abaki
felister
akuna real bila Ramos na hakuna Ramos bila real Madrid💪💪💪
Devotha
Mkataba wake ukiisha astaafu tu
lombo
gud newz asante
warda
Ila anakaa kwa wasi wasi sana #Meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Ramos jipemoyo ww mtu mkubwa usikae kwasiwasi Madrid bado upo jembe waho
Rehema
Huyo mshikaji jembe
Dorophina
Madrid hawawezi kumuachia Ramos ingawa umri umeenda
Johnmary joel
Tuwaachie viongozi wake#meridianbetz
Caroline
Ramos abaki Real Madrid
Emmy cleopa
Yuko vizur sana
Mariam mtandama
Habari mjema
isha
Ramos yupo vizuri
Theckla
Madrid cjui wanakwama wap mbona mshikaji yuko vizuri sana
Sadick
Ramos bado wamo na anahitajika kuendelea kutoa mchango Santiago lakini pia Club inatakiwa kuandaa warithi wa nguli huyu anayezeeka na utamu wake#meridianbettz
Amani
Hatima ya mwisho ni kumsikiliza wakala wake yeye ndo ambaye anaeyemtafutia mchongo#meridianbettz
Hope mwaikuka
Duh
Povel
Ramos wampe tu kandarasi mpya
Ester jackson
Yuko vizuri Ramos ila umri umeenda apumzike tu
Ernest
Ramos anastahili kumalizia soka lake pale na tena anastahili Heshima kwa kujitoa kwake juu ya Madrid.
Mwajuma
Ramso talent player
Theonestina
Ramos jeshi awezi kutoka
Magdalena
Madrid wanaanzaje kumpoteza kiungo muhimu na mahili kama Ramos
Agness
Abaki tuu asiondoke