Golikipa wa Inter Milan Yann Sommer ametangaza kustaafu soka la kimataifa baada ya kuisaidia Uswizi kufika robo fainali ya EURO 2024.

Sommer hataiwakilisha tena nchi yake katika ngazi ya kimataifa, akiwa amecheza mechi 94 za wakubwa.
Akiwa na umri wa miaka 36 mnamo Desemba na chini ya mkataba na Inter hadi Juni 2026, alitangaza habari hiyo kwa video ya kusisimua iliyofunika safari yake akiwa na jezi ya Uswizi.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

“Baada ya kutafakari kwa kina, nimeamua kusitisha kazi yangu kama golikipa wa timu ya taifa ya Uswizi. Ilikuwa heshima kubwa na bahati nzuri kuiwakilisha nchi yangu katika kiwango cha juu zaidi kwa miaka 12 na katika mechi 94 za kimataifa.” Aliandika kwenye Instagram.
Nia yangu sasa iko kwenye klabu yangu ya Inter Milan, ambapo bado nataka kupata mafanikio mengi. Alisema Sommer.
“Asante, Uswisi!”


