Kiungo wa Ivory Coast Franck Kessié amepewa ofa kwa klabu za Juventus na Atalanta, huku akitafuta kurejea Serie A baada ya misimu mitatu akiwa na Al-Ahli.

Juventus inaonekana kuwa mbele zaidi katika kinyang’anyiro hicho baada ya kocha Luciano Spalletti kuonyesha kumkubali mchezaji huyo kufuatia kiwango chake kizuri kwenye Taji la Dunia akiwa na Ivory Coast.
Kwa mujibu wa Tuttosport kupitia CalcioMercato, mawakala wa Kessié tayari wamewasiliana moja kwa moja na klabu zote mbili, huku Juventus ikimfuatilia kwa muda mrefu.
Uchezaji wake kwenye mashindano hayo, ikiwemo kufunga bao dhidi ya Ujerumani, umewakumbusha mashabiki wa soka Italia ubora wa mchezaji ambaye bado yuko kwenye hali nzuri ya kimwili licha ya kucheza Saudi Arabia.
Akiwa anapatikana bila ada ya uhamisho (free transfer), Kessié anataka mshahara wa kati ya €4 hadi €5 milioni kwa msimu, ambao ni chini sana ukilinganisha na takriban €14 milioni aliyokuwa akilipwa Al-Ahli.
Uhamisho wa kwenda Juventus unategemea wachezaji kuondoka kikosini, ambapo Carnevali atalazimika kupunguza idadi ya viungo wa kati kabla ya nafasi ya Kessié kuweza kupatikana.



