Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez amekiri klabu hiyo imekubali kushindwa kwenye mbio za taji la LaLiga, sasa wanajipanga kupigania ndoo ya Ligi ya mabingwa.
Sare 3 katika michezo yao tisa tangu La Liga irejee zimeigharimu Barca na kuwaruhusu Real Madrid kuwaondoa juu ya msimamo, huku kikosi cha Zinedine Zidane kikihitaji kushinda mchezo mmoja tu kutwaa Ubingwa.
Suarez ambaye alionekana kama atakosa msimu mzima uliobakia baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti mnamo mwezi Januari, lakini baada ya janga la corona kuongeza muda wa msimu kumalizika, imemsaidia yeye kupona na kurejea tena dimbani.
Huku nyota wa Kifaransa Antoine Griezmann akitarajiwa kukosa mechi mbili za kukamilisha msimu wa Ligi kwa Barcelona.
Suarez anatarajiwa kuanza katika mechi zote, lakini mshambuliaji huyo wa Uruguay amekiri kwamba kwa sasa wamejipanga kuweka nguvu yote kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Napoli Agosti 8.
“Ukweli ni kwamba kushinda ligi imekuwa ngumu,”- Suarez akiongea na Diario Sport.
“Tumepoteza nafasi ya ubingwa, dhidi ya Sevilla, Celta Vigo na Atletico Madrid. Bao la Aspas kwenye mchezo wa Vigo lilituumiza sana, kwani tulipoteza nafasi kubwa.
“Sasa lazima tujipange kwenye Ligi ya Mabingwa, ndio lengo letu.”
Goli la Griezmann katika mchezo wa kwanza dhidi ya timu ya gennaro Gattuso mwezi Februari liliwapa Barca faida ya bao la ugenini kabla ya mchezo wa kurudiana huko Camp Nou mwezi ujao.
Iwapo timu ya Quique Setien itawaondosha Wa-Italiano, basi watakabiliwa na Chelsea au Bayern Munich, katika mchezo wao wa robo fainali Ligi ya Mabingwa.
Unawaona Barcelona na Messi wakifika wapi katika Ligi ya Mabingwa, wanaweza kutwaa ndoo?
Kuna ofa kibao sana unazofaidi ikiwa unabashiri na Meridianbet. Jiunge sasa kufurahia ofa zetu
Bonyeza HAPA Kujiunga.
Magdalena
Suarez anachokisema ni kweli kabisa kama Barcelona imeshindwa kutetea taji la laliga itetee tu la ligi ya mabingwa Ili wasije wakakosa vyote
Elika
Mbona wanakata tamaa mapema..Suarez mnakosea wapi
Zeiyana
Habari mbaya kwa mashabiki wa Barcelona
Ester jackson
Poleni sana Barcelona sasa ndio muda wa kujipanga vingine .asante kwa nakala hii
felister
mnawavunja moyo mashabiki wenu jamani
Adelta
Poleni Sana Barcelona
Khadija
Habari mbaya kwa mashabiki wa livepool#meridianbettz
isha
Barcelona ni timu nzuri lakini sijui wanekosea wapi ila wasikate tamaa
Evaluziga
Barcelona Ni Tim nzuri sijui wanakosea wapi
lombo
🤣🤣 washaishiwa mipango uko clabu bingwa ndo kuna majesh kama yote pole yao
Fatina mfingi
Pole yao
Angelina
Poleni barcelona
Sylvester
Ni kweli Ubingwa kwao mwaka huu watausikia tu sababu Real Madrid naona washajihakikishia na hizo droo 3 zimewanyong’onyesha Barcelona kwenye mbio ya kulinyakua taji,wasubiri mwakani na wakijenge tena kikosi chake kwani wachezaji wake nyota wengi washachoka na umri umewatupa mkono
Genia Sikaluzwe
Wasikate tamaa mapema Barcelona waongeze juhudi iliwafike kwenye ubingwa
Tatu
Habari mbaya sana kwa mashabiki wa arsenal wajipange msimu ujao
Dorophina
Barcelona kwa sasa inashuka daraja wasipokuwa makini timu itayumba sana inabidi wajitahidi kurudisha heshima yao
Aziza mushi
Habari mbaya kwa mashabiki wa Barcelona.
Latifa juma mohamed
Daah Barcelona mnakata tamaa mapema, inabid wajikaze kwa msimu ujao
Tahiya
La liga ni ngumu sana kwa kwer
David Pere
Timu yao ishakuwa ya wazee tupu maana hakuna hata mchezaji mmoja mwenye umri chini ya miaka 33 wengi wao Ndio miaka hao jailsi
Fatuma kasomo
Barcelona mnakwama wapi?
farida ahmadi
Asikate tamaa Suarez nafasi pia Bado wanayo
Salma
Wasikate tamaa wajipe moyo
Zuhura omary kindamba
Barcelona ni timu nzuri ila cjui wanapotea wapi
Sadick
Baada ya Laliga kurejea niliona kila dalili kwamba Real Madrid imejiandaa zaidi kisaikolojia kuusaka Ubingwa wakati huo Barcelona kulikuwa na minong’ono ya kutokuwa na maelewano#meridianbettz
Samiah
Duuh
Flomena
Suarez ambaye alionekana kama atakosa msimu mzima uliobakia baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti mnamo mwezi Januari, lakini baada ya janga la corona kuongeza muda wa msimu kumalizika, imemsaidia yeye kupona na kurejea tena dimbani.
Franky
Longo lina bidi litimizwe so wana takiwa kujipanga tu game zilizo baki wafanye vizuri
devotha
Suarez alichokisema ni kweli lakini barcelona wamekosea kukata tamaa mapema ilibidi wajipe moyo na wapambane zaidi
Hope mwaikuka
Pambanen jaman
Gabriel
Suarez ameshazeeka huyo jamaa anatakiwa astafu hana jipya soka limeshamtuma maana kwa mashabiki tunaona uwezo Kwanza ushapungua ata akilalamika kuwa kulikuwa na ugumu
sabrina
Lazima akubali Real madrid sio ya mchezo mchezo
Issa
Barca wamepotea step sana toka kurudi kwa michezo na madrid kupata nafasi kuwapiku
Povel tz
Habar njema
Isaya massawe
Barcelona ni afadhali wawaze klabu bingwa maana kombe laligi msimu huu awawezi kuchukua
Amiri Kayera
Bado Barca inanafax kutwaaa
Saupha mohamed
Good news
Shafii
Mpinzani wake Madrid kila mechi kwake ni fainali hatuoni dalili za kupoteza mechi barca wanastahili kuangalia upande mwengine wa shilingi.
tumaini
Maoni:Mbona wanakata tamaa mapema
Frank Patrick
Msimu huu League ya mabingwa haina visingizio
caroline
mbona unakua dhaifu sana
Lydia Emmanuel Magoti
Msimu huu league ya mabingwa Aina visingizio
Ernest
Barca walichezea shilingi kwenye tundu la choo sasa wataambulia patupu
Furahav
Barca msimu huu hawana chao laliga.
Njiku
Nikweli kabisa ubingwa kwa barca ni mgumu sana labda wajipange dhidi ya uefa champions ligi
Samira
Barcelona kutokua na maelewano ndio kumewakwamisha kutwaa taji msimu huu
Omary lukumbi
Luis Suarez anachosema ni sahihi kabisa
Theckla
Suarez yuko sahihi
mwakalosi
zidane again and again
Rehema
Pole yao
warda
Suarez mnyama#