Mbeligiji Sven Vandenbroeck, amefunguka kuwa amekoshwa na viungo wake Ibrahim Ajibu, Hassan Dilunga na Said Ndemla ambao walifunga mabao kwenye mechi yao dhidi ya Mwadui FC kwa kubainisha wazi hiyo inaonyesha hamtegemei mtu mmoja kwenye suala la kufunga.
Mbelgiji huyo ameongeza kuwa mabao ya viungo hao yanamfanya sasa kuona timu yake ina uwezo wa kupata pointi kwa kufunga bila ya kuwategemea washambuliaji wao ambao walikosekana kwenye mechi kadhaa nyuma kutokana na majeraha.
Ajibu, Dilunga na Ndemla walifunga mabao wakati Simba ikishinda mechi yake ya ligi kuu mbele ya Mwadui FC kwa mabao 5-0 katika Uwanja wa Uhuru, Oktoba 31. Mabao mengine ya Simba yalifungwa na John Bocco aliyefunga mawili na Hassan Dilunga.
Sven amesema kuwa kitendo cha wachezaji hao kufunga kinampa wigo wa kuona wana uwezo wa kupata mabao na pointi kwenye mechi yoyote bila ya kuwategemea washambuliaji wake halisi ambao kwa sasa ni wagonjwa.
“Kila mmoja anaweza kufunga mabao hapa wala siyo kuwategemea Bocco, Kagere au Mugalu pekee. Ndemla, Dilunga wamefunga, ni jambo zuri na hii inafanya tuwe na mifumo mingi ya kucheza na tukapata mabao.
“Kocha anaweza kumpenda mshambuliaji anayefunga mabao 15 kwa msimu lakini siku ambayo akikamatwa na wapinzani timu haitafunga, hivyo kwa namna hii ya kila mtu kufunga inanifanya niwe na mbinu mbadala za kupata pointi,” alimaliza Mbelgiji huyo.
Hii ni halisi kwa ajili ya mashujaa wote! Ukiwa jasiri unavuna mkwanja kibao hapa na sloti hii ya Huangdi Casino. Waka nusu tukupe maradufu!
Dorophina
Simba wanaviungo wazuri sana
Adelta
Simba kwa sasa wako vizuri mashabiki tunafurahia
Ester jackson
Wote tunajua kuwa simba wanawachezaji vizuri ambao hawategemee mchezaji yoyote kwenye timu yao
Khadija
Simba wapo vzr sana
Elika
Safi sana mpaka kocha kasema hivyo ujue amewaelewa
Caroline
Ha ha ha simba bwanaa
Angelina
Hao ndo simba hawana kazi mbovu
Lydia Emmanuel Magoti
Kweli kabisa yupo sahii ndiocho kitu kinacho takiwa kutomtegemea mtu kufunga kwasababu mtu yoyote akiwa amekaa vizuri nagoli lazima afunge nasio kumtegemea mtu kwenye mechi mfungaji malufu ndio afunge inakuwa siopoa kwai akitoke yulemfungaji Kama ayupo kwai magoli ayafungwi lakini kwasimba tunaviungo makini Sana nawafungaji Kama ote naikubali Sana simba
Salma ngende
Kumbe
Tatu
Ila kikosi cha simba kipo imara mambo yote tarehe7 pale kwa mkapa
Sauda
Simba kuna majembe
Saupha mohamed
Simba bigwaa
aisha
Simbaaaaaa wako vizuri sana
Sabrina
Imeisha hiyoooo
Mwajumah
Simba wapo vizuri sana
Fatina mfingi
Simba baba lao uwa hatunag maneno mengi sie!
zeiyana
Ibrahim hana maajabu yoyote
Shani
Simba imara
Hopemwaikuka
Hao watu ni nomaa
Issa
Asiw na presha angoje kipigo tu kweny kkoo derby
Povel
Mambo ni moto kuelekeah Kariakoo DERBY
warda
Huyu Seven dawa yake ipo jikon