Sven: Lazima Wachezaji Wajitume Tupate Matokeo

Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck raia wa Ubelgiji amecharuka na kuwataka wachezaji wake kucheza kwa kujituma kuelekea kwenye mchezo wa marudio wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya FC Platinum.

Simba ilipoteza mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya FC Platinum uliochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimbabwe kwa kufungwa bao 1-0 lililopachikwa na Perfeck Chikwende.

Ina kibarua cha kupindua meza Uwanja wa Mkapa unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa Januari 6, ambapo Ofisa Habari wa timu hiyo Haji Manara amesema kuwa utakuwa ni mchezo wa vita ndani ya Dar.

Vandenbroeck amesema kuwa kilichowaponza washindwe kushinda mchezo huo ni kukosekana kwa umakini kwa wachezaji wake jambo ambalo limemkasirisha hasa hivyo hatapenda kuona makosa yanajirudia.

 

“Tuliweka wazi malengo yetu tangu awali kwamba ni lazima tuweze kutinga hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika. Kuanza kwa kupoteza hiyo ni mbaya kwetu na haijanifurahisha hasa kwa kuwa mchezo tuliweza kuumiliki ila umakini ulikosekana.

“Kwenye mchezo wetu wa marudio hatuna chaguo la kufanya zaidi ya kutafuta matokeo chanya na wachezaji kujituma zaidi, hivyo mashabiki watupe sapoti tunaamini kwamba tutafanya vizuri,” amesema Vandenbr.oeck.


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?

SOMA ZAIDI

 

15 Komentara

    Simba washaanza kuwa mdebwedo

    Jibu

    Simba inazingua sana

    Jibu

    Kweli yupo sahii

    Jibu

    Simba inazingua kinoma

    Jibu

    Wakazee

    Jibu

    Makini sana

    Jibu

    Bila kujituma huwezi fanikiwa

    Jibu

    Wakaze tupate ushindi

    Jibu

    Nikweli simba wajitume ili wampate ushindi

    Jibu

    Kabsaa wakaze

    Jibu

    Yuko sahihi

    Jibu

    Yuko makini san

    Jibu

    Yupo makini sanaa kiukweli

    Jibu

    Kujituma ni muhimu sana katika soka kwahiyo simba wasijibweteke

    Jibu

Acha ujumbe