Tadeo Lwanga Katika Fikra za Claudie Makelele

Nililazimika kuusubiri usiku wa saa nane ili niweze kutafakari kwa utulivu zaidi, nililazimika kuusubiri mchana wa saa nane ili nipate wasaa wa kuandika vema zaidi, Nililazimika kuisubiri jioni ya saa kumi niweze kuachilia hili andiko.

Si shairi la mahaba, la! Si muendelezo wa makala niliyoipotezea siku za nyuma, la! Si sehemu ya riwaya yangu ya Nisamehe dunia, la! Si maoni yangu juu ya mabao manne ya Olivier Giroud usiku wa jana, la! Ni juu ya mganda aliyetua Unyamani, Taddeo Lwanga.

Taarifa kutoka kwa vyanzo ninavoviamini vinadai, Taddeo alivunja mkataba na klabu yake ya Misri, walishindwa kumlipa mshahara kwa muda mrefu. Na si alitemwa kama inavodaiwa, si alifeli kama inavodaiwa. Maslahi bwana! Nipe muda kidogo nikuambie kitu kumuhusu Claudie Makelele.

Mwaka 2003, Real Madrid iliyosheheni Galacticos ilitwaa la liga. Ndani ya kikosi alikuwepo Claudie Makelele. Msimu ulipoisha alimfuata rais Florentino Perez ofisini na kumuambia, kocha Vicente del Bosque ameniambia bado ananihitaji kwa muda mrefu, tunaweza kujadili mkataba mpya?

Perez alitabasamu akamuambia, “tutakupa mkataba mpya, japo hautafanana na Zidane lakini utakuwa mnono zaidi ya huu wa sasa”. Makelele hakujalisha, alichoridhika ni kwamba atabaki Real Madrid kwa maslahi zaidi. Perez akampa mkono akamuambia, nenda ukafurahie likizo yako.

Makelele alirejea kutoka likizo akijua ana miaka minne zaidi Madrid, lakini haikuwa hivo. Perez alimuambia klabu imetumia pesa nyingi kumsajili David Beckham, hivo hamna pesa ya kumlipa, kama Makelele anataka asaini mkataba bure kwa sababu Real Madrid ni timu ya ndoto ya kila mchezaji.

Makelele alikataa akaamua kujiunga na Chelsea, kwake mpira haukuwa burudani, mpira ulikuwa kazi, mpira ulikuwa baba na mama kwake. Kivipi asaini mkataba wa bure kisa ya mafanikio ya jina? Alienda Chelsea na mpaka leo wanakiri London Magharibi hawajawahi kumuona kiungo mkabaji kama Claudie. Ameshinda mataji kibao pale, ana heshima kubwa sana pale.

Itazame tena picha ya Taddeo kisha uniulize, kwanini ameondoka Misri? Nitakuambia amefuata njia ya Claudie Makelele. Maslahi bwana!


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

22 Komentara

    Tunasubiri kuona maajabu yake

    Jibu

    Vizuri Sana atimae kitu ukitakacho kishatimia

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Tunasubiri kwa hamu

    Jibu

    Game ya kibabe

    Jibu

    Asnt kwa taarif meridianbet

    Jibu

    Watazamaji tunasubilia vitendo tu

    Jibu

    Game ya kibabe

    Jibu

    Game ya kiwango chake

    Jibu

    Game bombs

    Jibu

    Gemu ya kijanja

    Jibu

    Simba wamepata mnyama kama wenyewe

    Jibu

    saf

    Jibu

    Jambo zuri kwa Wana Simba.

    Jibu

    Karibu Lwanga kwenye timu ya mabingwa nchini

    Jibu

    Mechi mzur

    Jibu

    Duuh acha tuone makeke yake

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Mtanange wa kibabe

    Jibu

    Karibu nyumbani

    Jibu

    Tumewapata kwa taarifa nzuri

    Jibu

Acha ujumbe