Nililazimika kuusubiri usiku wa saa nane ili niweze kutafakari kwa utulivu zaidi, nililazimika kuusubiri mchana wa saa nane ili nipate wasaa wa kuandika vema zaidi, Nililazimika kuisubiri jioni ya saa kumi niweze kuachilia hili andiko.
Si shairi la mahaba, la! Si muendelezo wa makala niliyoipotezea siku za nyuma, la! Si sehemu ya riwaya yangu ya Nisamehe dunia, la! Si maoni yangu juu ya mabao manne ya Olivier Giroud usiku wa jana, la! Ni juu ya mganda aliyetua Unyamani, Taddeo Lwanga.
Taarifa kutoka kwa vyanzo ninavoviamini vinadai, Taddeo alivunja mkataba na klabu yake ya Misri, walishindwa kumlipa mshahara kwa muda mrefu. Na si alitemwa kama inavodaiwa, si alifeli kama inavodaiwa. Maslahi bwana! Nipe muda kidogo nikuambie kitu kumuhusu Claudie Makelele.
Mwaka 2003, Real Madrid iliyosheheni Galacticos ilitwaa la liga. Ndani ya kikosi alikuwepo Claudie Makelele. Msimu ulipoisha alimfuata rais Florentino Perez ofisini na kumuambia, kocha Vicente del Bosque ameniambia bado ananihitaji kwa muda mrefu, tunaweza kujadili mkataba mpya?
Perez alitabasamu akamuambia, “tutakupa mkataba mpya, japo hautafanana na Zidane lakini utakuwa mnono zaidi ya huu wa sasa”. Makelele hakujalisha, alichoridhika ni kwamba atabaki Real Madrid kwa maslahi zaidi. Perez akampa mkono akamuambia, nenda ukafurahie likizo yako.

Makelele alirejea kutoka likizo akijua ana miaka minne zaidi Madrid, lakini haikuwa hivo. Perez alimuambia klabu imetumia pesa nyingi kumsajili David Beckham, hivo hamna pesa ya kumlipa, kama Makelele anataka asaini mkataba bure kwa sababu Real Madrid ni timu ya ndoto ya kila mchezaji.
Makelele alikataa akaamua kujiunga na Chelsea, kwake mpira haukuwa burudani, mpira ulikuwa kazi, mpira ulikuwa baba na mama kwake. Kivipi asaini mkataba wa bure kisa ya mafanikio ya jina? Alienda Chelsea na mpaka leo wanakiri London Magharibi hawajawahi kumuona kiungo mkabaji kama Claudie. Ameshinda mataji kibao pale, ana heshima kubwa sana pale.

Itazame tena picha ya Taddeo kisha uniulize, kwanini ameondoka Misri? Nitakuambia amefuata njia ya Claudie Makelele. Maslahi bwana!
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!




Magdalena
Tunasubiri kuona maajabu yake
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana atimae kitu ukitakacho kishatimia
Caroline
Asante kwa taarifa
Sauda
Tunasubiri kwa hamu
Issa
Game ya kibabe
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
Dorophina
Watazamaji tunasubilia vitendo tu
Shakila mrope
Game ya kibabe
Adelta
Game ya kiwango chake
Saupha mohamed
Game bombs
Zainabu kihongosi
Gemu ya kijanja
Samira
Simba wamepata mnyama kama wenyewe
lombo
saf
Shafii
Jambo zuri kwa Wana Simba.
Sadick
Karibu Lwanga kwenye timu ya mabingwa nchini
Mariam mtandama
Mechi mzur
Fatina mfingi
Tunasubir tuone maajab uwanjan
aisha
Duuh acha tuone makeke yake
Khadija
Safi sana
neema hassan
Mtanange wa kibabe
Tatu
Karibu nyumbani
warda
Tumewapata kwa taarifa nzuri