Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag inaelezwa amewavutia mabosi wote wanaoitaka klabu hiyo kutokana na mwenendo wake ndani ya klabu hiyo tangu aichukue tiimu hiyo mwaka jana mwezi Juni.
Mabosi wawili wanaoiwania klabu hiyo Sheikh Jassim kutoka Qatar na Sir Jim Ratcliff raia wa Uingereza wote wanaelezwa kuvutiwa na Ten Hag, Hivo mmoja wao akichukua timu ataendelea kuweka imani yake kwa kocha huyo ambaye anaonekana kufanya vizuri klabuni hapo.Kocha huyo wa kimataifa wa Uholanzi amekua akionesha mabadiliko makubwa ndani ya timu hiyo tangu kuchukua timu hiyo mwezi Juni mwaka jana, Akifanikiwa kuitengeneza timu hiyo na kuifanya kua moja ya timu bora kwasasa nchini Ulaya na kuingia ndani ya timu nne za juu mpaka sasa ikikamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.