Felix Auger-Aliassime amefunga sehemu ya ukurasa mkubwa wa maisha yake ya tenisi baada ya kuachana na kocha wake wa muda mrefu, Frederic Fontang, mara tu baada ya kupoteza kwa Novak Djokovic kwenye robo fainali ya Wimbledon, mechi iliyodumu saa tano na dakika 15, ndefu zaidi katika historia ya robo fainali za mashindano hayo. Baada ya miaka 10 ya ushirikiano, Auger-Aliassime alitoa ujumbe wa hisia kwa Fontang, akimshukuru kwa mchango wake katika safari yake ya kufika kileleni.

Fontang, akizungumza na L’Equipe, alifichua kwamba walikuwa wamepanga ama kuongeza mtu mpya kwenye benchi au kuachana mwishoni mwa 2025 iwapo matokeo hayangekuwa mazuri. Lakini kwa kuwa Felix alimaliza msimu uliopita akiwa namba tano duniani, waliamua kuendelea. Hata hivyo, baada ya kupoteza kwa Flavio Cobolli kwenye Roland Garros na kisha Djokovic Wimbledon, walikubaliana kumaliza safari yao kwa heshima.
Kwa sasa Auger-Aliassime yupo nafasi ya nne duniani, akiwa na rekodi ya kufika robo fainali kwenye Grand Slam zote na Masters 1000, pamoja na nusu fainali mbili za Grand Slam. Kile kilichokosekana ni taji kubwa la Grand Slam, hatua ya mwisho ya ubora. Mwaka huu, safari yake imekuwa na changamoto, alilazimika kujiondoa raundi ya kwanza Australian Open kwa sababu ya cramp, kisha akapoteza nafasi ya dhahabu Roland Garros baada ya Sinner kutolewa mapema, na Wimbledon akakaribia kumtoa Djokovic.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Sasa macho yote yameelekezwa kwenye US Open, nafasi yake ya mwisho ya mwaka huu kutafuta taji la kwanza la Grand Slam. Hapo ndipo Auger-Aliassime atajaribu kuandika historia mpya bila Fontang pembeni, akijaribu kuthibitisha kwamba anaweza kupiga hatua ya mwisho ya ubora.

Hii ni hadithi ya mabadiliko, kocha na mchezaji wanaachana baada ya mafanikio makubwa, lakini safari ya bingwa bado inaendelea. US Open inaweza kuwa jukwaa la kuonyesha kama Auger-Aliassime anaweza kugeuza maumivu ya kupoteza kuwa ushindi wa kihistoria.


