Daniil Medvedev Bingwa ATP Finals 2020

Mashindano ya ATP Finals 2020 yamemalizika na Daniil Medvedev ameumaliza mwendo kwa kubeba taji kubwa zaidi kwenye maisha yake ya uchezaji tenesi mpaka sasa.

Fainali ya ATP 2020 ilimkutanisha Medvedev dhidi ya Bingwa wa US Open 2020 – Dominic Thiem katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa O2 Arena jijini London – Uingereza.

 Daniil Medvedev ameshinda mchezo wa fainali kwa matokeo ya seti 4-6 7-6 (7-2) 6-4. Licha ya Thiem kuongoza kwenye seti ya 2, Medvedev alipambana kuzitafuta pointi 7 katika seti ambayo ilipelekea kuchezwa seti ya ziada ili kumpata mshindi.

Ubingwa wa ATP Finals 2020, unamfanya Daniil Medvedev kumaliza mwaka akiwa nafasi ya 4 kwa ubora duniani.

Medvedev anakuwa mchezaji wa kwanza kuwafunga wachezaji watatu bora duniani katika shindano moja. Aliwafunga Novak Djokovic na Rafael Nadal. Hakuwa amemfunga mchezaji yeyote aliyepo kwenye 10 bora tangu November 2019 mpaka Oktoba 2020, sasa amewafunga wachezaji 7 ndani ya wiki 4.

Mashindano ya ATP Finals yamefanyika Uingereza kwa mara ya mwisho, kuanzia 2021 mashindano hayo yatakuwa yakifanyika jijini Turin – Italia.


USICHELEWE KUKAMATA MKWANJA HUU!

Hadi 130,000,000 Tsh kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.

Meridianbet Tanzania Casino

SOMA ZAIDI

12 Komentara

    Hongera sana Daniil

    Jibu

    goodupdate

    Jibu

    Safi san

    Jibu

    Saginaw sana

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    pongezi kwake

    Jibu

    Congar medvedved👏👏

    Jibu

    Congratulations kwake

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Good

    Jibu

    Hongera yake

    Jibu

Acha ujumbe