Bingwa namba 1 kwa ubora duniani (kwa wanawake), Ashleigh Barty, amefuzu hatua ya fainali kunako mashindano ya Madrid Open 2021.
Barty amefanikiwa kutua hatua ya fainali baada ya kumfunga Paula Badosa kwa seti 6-4 6-3. Kumfunga Badosa kunakamilisha jumla ya wapinzani 30 walioambulia kipigo kutoka kwa Barty katika safari yake ya kufikia hatua ya fainali kunako Madrid Open.

2019, Barty aliibuka kidedea kwa kubeba taji la French Open na hakurejea tena uwanjani kwa miezi 11 kutokana na mlipuko wa COVID19 mpaka mwezi Aprili 2021 ambapo aliibuka kidedea kwenye mashindano ya Stuttgart Open.
Ashleigh Barty atachuana na Anastasia Pavlyuchenkova au Aryna Sabalenka kwenye fainali ya mashindano hayo. Baada ya kuulizwa kama ataangalia mchezo wa nusu fainali ya pili (Pavlyuchenkova vs Sabalenka), Barty amejibu, “mimi sio mfuasi wa muda wa kihispania. Mimi ni raia wa Australia. Ninalala mapema, ninaamka mapema.”
TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO
Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!
Pongezi nyingi kwake
Inapendeza ongera zao
Hongera yake
Good.
.good paformance