Habari mbaya kwa mashabiki wa mchezo wa tenesi. Rodger Federer atayakosa mashindano ya Australian Open kwa mara ya kwanza baada ya miaka 22.
Rodger Federer bado anaendelea na matibabu baada ya kufanyiwa upasuaji mara mbili akiwa nje ya uwanja toka mwezi Januari 2020.
Federer alitarajia kurejea uwanjani kwenye mashindano ya Australian Open ambayo yamesogezwa mbele mpaka Februari 8, lakini kutokana na afya yake atashindwa kuhudhuria mashindano hayo.
Federer ameshiriki mashindano ya Australian Open kwa miaka 21 mfululizo lakini kutokana na hali yake, wakala wa bingwa huyu wa Grand Slam mara 20 amesema “ni uamuzi sahihi utakaoleta matokeo chanya ya muda mrefu.”

Taarifa rasmi kutoka kwa mkurugenzi wa Melbourne – Craig Tiley amesema, ” Rodger yupo nyuma ya muda kwa ushiriki wake kwenye mashindano ya Grand Slam”.
Mchezo wa mwisho kwa Federer ilikuwa ni nusu fainali ya Australian Open ambapo alipoteza kwa bingwa wa mwaka huu (2020) – Novak Djokovic.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Dorophina
Pole sana federer
Adelta
Pole Sana federer mwenyezi mungu amfanyiye wepesi apone majeraha alinayo ili arudi kwenye hali yake ya zamani
Rahmal
Federer pole sana
Hopemwaikuka
Bila Nadal mashndano yatapoa sana
Sarah
Pole yake
Angelina
Sad news
Tatu
Pole sana
Lydia Emmanuel Magoti
Duu pole yake
Issa
Federer ni noma sana
warda
pole yake