Mambo yamemuendelea kombo bingwa mtetezi (wanawake) wa Australian Open, Sofia Kenin. Ayaaga mashindano mapema huku Ashleigh Barty akiendelea kusonga mbele.
Kenin amejikuta akitaabika dhidi ya mpinzani wake, Kaia Kanepi walipokutana pale Margaret Court Arena. Ndani ya saa1 na dakika 4, Kenin alipigwa seti zote kwa matokeo ya 6-3 6-2.
Kwa matokeo haya, Kanepi atachuana na Donna Vekic katika mzunguko wa tatu wa mashindano ya Australian Open 2021.
Katika mchezo mwingine, bingwa namba 1 wa dunia – Ashleigh Barty alimlaza na viatu mpinzani wake, Daria Gavrilova kwa matokeo ya seti 6-1 7-6 (9-7).
Barty atachuana na Ekaterina Alexandrova katika mchezo wa mzunguko wa tatu.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Sadick
Nataka kuona Naomi akifanya vzr kwenye mashindano haya yenye heshima kubwa
Adelta
Naomi Yuko vizuri mashindano yazima ashinde
Caroline
Hongera sana Sofia
Magdalena
Safi Sana Sophia
Samira
Naomi yupo vizuri sana
Mwanahamisi
Safi sana
Neema juma
Naomi najua yuko vizuri sana
warda
Imekaa poa