Tetesi za Soka Barani Ulaya.


Tetesi zinasema mshambuliaji wa Leeds United raia wa Uhispania Rodrigo, 30, amekanusha uvumi kuwa hana furaha Elland Road na kwamba anataka kurejea La Liga.

Tetesi zinasema mshambuliaji wa Boca Juniors Tevez, 37, ambaye ana miezi 12 kuamua ikiwa ataendeleza mkataba wake na mabingwa wa Argentina baada ya msimu huu, anahusishwa na kuhamia Marekani.

Nuremberg ina panga kumsajili beki wa kati wa Huddersfield Town Christopher Schindler, 30, mkataba wake na Ujerumani utakapokamilika msimu huu.

 

Kocha wa Burnley Sean Dyche anaonekana kuwa mgombea ambaye anaongoza kuwa katika kinyanganyiro cha kumtafuta kocha mpya wa Crystal Palace ikiwa Roy Hodgson, 73, hataongeza mkataba wake baada ya msimu huu.

Manchester United iko tayari kutoa ofa kwa kiungo wa kati, raia wa Uholanzi, 23, Donny van de Beek ya kumuuza Juventus kama sehemu ya makubaliano ya mabadilishano ya kumsajili mchezaji wa kimataifa raia wa Ufaransa Adrien Rabiot, 25.

Tetesi zinasema Burnley inapanga jinsi ya kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 10 kwa mlinzi wa Middlesbrough ambaye pia alikuwa katika timu ya England Under-21 Dael Fry, 23.

 

Mlinzi wa Italia Giorgio Chiellini yuko tayari kusalia Juventus hata baada ya mkataba wake kukamilika msimu huu, amesema ajenti wake Davide Lippi, lakini klabu ya Turin bado haijampa mkataba mpya.

Tetesi zinasema Real Madrid imekataa ofa ya Tottenham baada ya klabu hiyo ya London kutaka kumsajili mlinzi wake raia wa Uhispania, 19, Miguel Gutierrez.


UNAWEZAJE KUKOSA KASINO YA BREAK AWAY LUCKY WILDS INAYOKUPA NAFASI YA USHINDI MURUA.

Break Away Lucky Wilds ni moja ya Sloti pendwa katika kasino za #meridianbet inayokupa mara 11,000X ya dau lako, unayo nafasi ya kuwa milionea unasubiri nini?

CHEZA HAPA

5 Komentara

    Asanteni kwa taarifa

    Jibu

    Zipo poa

    Jibu

    Zinasomeka

    Jibu

    Nice update

    Jibu

    Zilikuwa poa sna

    Jibu

Acha ujumbe