Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, Chelsea wako tayari kutoa wachezaji kadhaa, pamoja na mshambuliaji wa England Tammy Abraham, 23, na kipa wa Uhispania Kepa Arrizabalaga, 26, katika ofa ya kubadilishana wachezaji pamoja na pesa ili kupata sahihi ya mshambuliaji wa Tottenham na Uingereza Harry Kane.

Tetesi zinasema, Mlinzi wa Arsenal Sead Kolasinac, 27, anatarajiwa kuondoka klabuni humo msimu huu wa joto, na Schalke na Lazio wakiwa mstari wa mbele kumtafuta mchezaji huyo wa kimataifa wa Bosnia na Herzegovina.

Manchester City watafungua mazungumzo ya mkataba mpya na Raheem Sterling msimu huu wa joto licha ya mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 26 kupoteza nafasi yake katika kikosi katika wiki za hivi karibuni.

 

raheem sterling

Arsenal na Aston Villa wameongeza tena hamu yao kumsajili mchezaji wa Norwich mwenye umri wa miaka 24, Emiliano Buendia, ambaye anathaminiwa kugharimu kati ya pauni milioni 35 hadi pauni milioni 40.

Tetesi zinasema, Real Madrid wana mpango wa kumsajili Paris-St Germain na mshambuliaji wa Ufaransa 22, Kylian Mbappe.

Wolves wanafanya mazungumzo na meneja wa zamani wa Benfica Bruno Lage juu ya kumrithi Mreno mwenzake Nuno Espirito Santo, ambaye ataondoka kilabuni humo baada ya mchezo wa Jumapili dhidi ya Manchester United.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Mshambuliaji wa Argentina Sergio Aguero, 32, amekubali mkataba wa miaka miwili kujiunga na Barcelona wakati mkataba wake wa Manchester City utakapomalizika mwishoni mwa msimu.

Tetesi zinasema Wolves wanamfuatilia Mreno Paulo Fonseca, ambaye ataondoka Roma msimu huu wa joto.

Mchezaji wa Tottenham aliye katika uhamisho wa mkopo Gareth Bale, 31, anafikiria kustaafu mkataba wake wa Real Madrid utakapomalizika mwishoni mwa msimu ujao.

Tottenham watajaribu kumshawishi bosi wa Leicester, Brendan Rodgers, 48, kuwa meneja wao mpya ikiwa wolves watashindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.

Tetesi zinasema Leeds wanatarajia kupokea ofa kwa mlinzi wa Uhispania mwenye umri wa miaka 27 Diego Llorente msimu huu wa joto lakini hawana nia ya kumuuza.

Leicester wanaongoza harakati za kumsajili mshambuliaji wa Celtic Odsonne Edouard, ingawa Arsenal, Newcastle na Aston Villa pia wanamtaka Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 23.

 

Tetesi zinasema, West Ham wanataka kusalia na mshambuliaji anayewachezea kwa mkopo wa Manchester United na England Jesse Lingard, 28.

Leeds wameanzisha mazungumzo na Manchester City juu ya mkataba wa kudumu wa kiungo wa kati wa Uingereza anayehudumu huko kwa mkopo Jack Harrison.

Kocha wa Swansea Steve Cooper na meneja wa zamani wa Huddersfield David Wagner ni miongoni mwa wanaowania nafasi ya Sam Allardyce klabuni West Brom.


UNAWEZA KUWA MILIONEA WAKATI WOWOTE!

Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.

kane, Kane Aweka Wazi Maazimio Yake Kucheza UEFA., MeridianbetBASHIRI SASA

2 Komentara

    Chelsea waangalie maamuzi yao

    Jibu

    Ziko poa tetesi

    Jibu

Acha ujumbe