Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, Manchester United bado wanawania saini ya mlinzi wa RB Leipzig na Ufaransa Nordi Mukiele, mwenye umri wa miaka 23.

Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa Chelsea na Ujerumani Timo Werner, 25, alitaka kujiunga na Manchester United kabla ya kuhamia Stamford Bridge.

Winga Mdenmark anayewindwa na Tottenham na Sampdoria mwenye umri wa miaka 21- Mikkel Damsgaard, pia anatafutwa na Juventus.

Tetesi zinasema, Arsenal watalazimika kulipa takriban pauni milioni 38.5 iwapo watataka kusaini mkataba na mshambuliaji Mmorocco Youssef En-Nesyri, 24.

 

Juventus wanaripotiwa kuwa watamuuza kiungo wa kati wa Wales Aaron Ramsey, 30 mwezi Januari huku klabu za West Ham, Everton na Newcastle zikimtaka.

Inter Milan imemjumuisha mlinda lango wa Arsenal na Ujerumani Bernd Leno, 29 katika orodha ya wachezaji wanaowalenga kuwasajili katika dirisha lijalo la usajili.

Tottenham wanangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa kati Juventus na Sweden mwenye umri wa miaka 21 Dejan Kulusevski katika dirisha dogo la mwezi January.

 

Tetesi zinasema, Chelsea wako tayari kumuuza kiungo wa kati Mfaransa mwenye umri wa miaka 30 N’Golo Kante msiumu ujao.

Tetesi zinasema Chelsea wanajiandaa kupeleka dau jipya kwa ajili ya kumsajili winga wa Italia Federico Chiesa.

Mlinzi wa Leicester City na Uturuki Caglar Soyuncu, mwenye umri wa miaka 25, ni mmoja wa wachezaji wanaotafutwa na Real Madrid.


FUNGA BAHATI YAKO NA MERIDIANBET.

Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe