Tetesi zinasema Arsenal wanakaribia kukamilisha mchakato wa uhamisho wa Gabriel Magalhaes. Gunners wametoa ofa ya mkataba wa miaka mitano, kumpata beki huyo aliye na umri wa mika 22 raia wa Brazil.
Tetesi zinasema Napoli wakimkosa Gabriel, huenda wakamnunua beki Arsenal Mjerumani Shkodran Mustafi.
Tetesi zinaarifu Manchester United pia wako mbioni kumsaka Gabriel, lakini lazima waongeze ofa yao kumpata.

Manchester United wametoa ofa ya £27m kumnunua winga wa Juventus na Brazil Douglas Costa, 29, lakini klabu hiyo ya Serie A inataka kulipwa £9m zaidi.
Chelsea wanakaribia kumpata winga wa Ujerumani Kai Havertz ,21, baada ya kufanya mazungumzo zaidi na Bayer Leverkusen kuhusu bei yake.
West Ham wanajaribu kumuuza kiungo wa kati wa England Jack Wilshere, 28, na wako tayari kulipa mwaka mmoja uliosalia katika mkataba wake ama kupunguza ada ya kumwezesha kuhamia klabu nyingine.

Chelsea wameongeza juhudi za kumsaka nahodha wa Paris St-Germain Thiago Silva, huku beki huyo wa mwenye umri wa miaka 35- wa Brazil akiwa tayari kucheza Jumapili katika finali ya Champions League dhidi ya Bayern Munich siku ya Jumapili.
Tetesi zinasema Kipa wa Lille Mike Maignan, 25, ananyatiwa na Chelsea.
Tetesi zinasema Manchester City wameafikiana na Napoli kuhusu usajili wa beki wa Senegal Kalidou Koulibaly, 29.
Wachezaji wenza wa Jadon Sancho katika klabu ya Borussia Dortmund wana imani nyota huyo wa England mwenye umri wa miaka 20 ambaye amehusishwa na uhamisho wa kwenda Manchester United atasalia katika klabu hiyo ya Bundesliga kwa mwaka mwingine mmoja baada ya kushiriki mazoezi ya kabla ya kuanza kwa msimu.

Paris St-Germain inamnyatia beki wa Manchester United na Ureno Diogo Dalot, 21.
Liverpool inafikiria kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich Thiago Alcantara huku mchezaji huyo wa Uhispania, 29, akipatikana kwa pauni milioni 30.
Kocha mpya wa Barcelona Ronald Koeman anataka kumleta kiungo wa kati wa Liverpool na Uholanzi Georginio Wijnaldum, 29, Nou Camp.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Ester jackson
Usajili Wa Chelsea msimu huu wanaongoza kusajili wachezaji wenye uwezo Wa juu sana
Mwajumah
Chelsea msimu huu wanafanya usajili wa wachezaji wenye uwezo mzuri uwanjan naona wanataka kikosi bora zaid#Meridianbettz
Adelta
Arsenal wafanye mchakato ili waweze kumchukuwa huyo beki@meridianbettz
Khadija
Msimu huu wanafanya usajili wa wachezaji wenye uwezo#meridianbett
Dorophina
Arsenal wafanye araka wamsajili Gabriel Mambo yaende sawa maana Gabriel yupo vizuri sana
Sadick
Bado klabu nyingi zinasuasua kwenye usajiri,tetesi zimekuwa nyingi kuliko matendo#meridianbettz
Ernest
Arsenal washafanya yao kwa Gabriel Magalhaes
Nasra
Arsenal wafanye uchaguzi mzuri sasa
Zeiyana
Arsenal kama wataikosa sain ya Gabriel si mbaya wakimchukua mustafi yupo vizuri tu bado kiwango chake akijashuka
Mwanahamisi
Chelsea msimu huu wafanye usajili mzuri wa wachezaji
Sauda
Chelsea wanataka kikosi kilicho bora
Caroline
Klabu nyingi zinasua kusajili
aisha
Arsenal wamepata jembee kumpata gabriel maana usajili wao hawakosea kwasababu kijana yuko vizuri
felister
mbona kitambo tu arsenal washafanya yao
De paschal
Chelsea wafanye kwel siyo kuleta story tu zw utetezi tu
Lydia Emmanuel Magoti
Chelsea fanyeni kweli sio polojo mdomoni tuu
Fatuma kasomo
Tetesi zimekua nyingi kuliko matendo
Issa
Manchester imchukue douglas costa itakuwa safi sana
JULIANA
Asante kwataharifa
Sabrina
Arsanal wakimpata Gabriel itakua Poa sana
Amiri Kayera
Arsenal wakamilish uyu mchezaji mzur san
jullie
hizi tetesi ziko vizuri
Hope mwaikuka
Timu zote zmejtahid kwa kusajl wachezaj wazur
Saupha mohamed
Habari njema
Samira
Imekaa poa hii
Shafii
Tetesi ziko vizuri.
warda
Wawoo wesha fanikiwa
magdalena
united waweke dau mezani wamchukue uyo winga yupo vizuri
Salma ngende
Kocha mpya wa Barcelona akaze awachukue so jamaa
Gabriel
EPL inaushindan mkubwa sana kiukwel katika msimu wa usajil atashindwa ajiandae kombe kuangalia
Rose kapinga
Mambo ya soka hayoo!!!
David Pere
Bado klabu nyingi zinasuasua kwenye usajiri,tetesi zimekuwa nyingi kuliko matendo