Tetesi zinasema Paris St-Germain na Manchester United wanapigiwa upatu kumsajili Lionel Messi baada ya mshambuliaji huyo wa Argentina, 33, kuifahamisha Barcelona kwamba anataka kuondoka, wako tayari kulipa ada ya kumpata.
Barua iliotumwa na klabu hiyo siku ya Jumanne inasema kwamba anataka kutumia kifungu kilichopo katika kandarasi yake ili kuweza kuondoka katika klabu hiyo akiwa mchezaji huru mara moja.
Barcelona ilifungwa magoli 8-2 na klabu ya Ujerumani ya Bayern katika robo fainali ya kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya mnamo tarehe 16 Agosti.
Barcelona hata hivyo inaamini kwamba kifungu hicho kilipitwa na wakati na kwamba kandarasi ya Messi katika klabu hiyo itakamilika 2021 huku kukiwa na kifungu cha Yuro milioni 700 kwa klabu yoyote inayotaka kumnunua.
Thiago Silva, 35, yuko tayari kufanyiwa vipimo vya matibabu na Chelsea siku ya Alhamisi, licha ya jaribio la dakika za mwisho za Paris St-Germain kutaka kumpatia mkataba mpya mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil.
Philippe Coutinho angelipendelea kurejea katika Ligi ya Epl badala ya Barcelona huku Manchester United, Arsenal na Chelsea wakimnyatia nyota huyo wa Brazil aliye na umri wa miaka 28.
Everton wako kwenye mazungumzo ya kumsaini kiungo wa kati wa Real Madrid James Rodriguez, 29, baada ya mkufunzi Zinedine kuonesha ishara ya kumtaka aondoke klabu hiyo.
Chelsea wanakaribia kukamilisha mchakato wa kumsajili mlinzi wa zamani wa Nice Malang Sarr, 21, kwa mkataba wa miaka mitano.
Kiungo wa kati wa Ajax Donny van de Beek yuko tayari kuhamia Ligi ya Epl msimu huu wa joto huku Manchester United wakiwa mbioni kumsaka Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 23.
Tetesi zinasema Newcastle United wanamtaka mchezaji wa safu ya kati na nyuma wa Arsenal Rob Holding, 24, kwa mkopo na Gunners wako tayari kupokea ofa.
Tetesi zinasema AC Milan wanapania kumsajili kiungo wa kati wa Real Madrid Mhispania Brahim Diaz, 21, kwa mkopo msimu wa 2020-21.
Crystal Palace wamekubali kulipa £14m kumnunua kiungo wa kati wa QPR Eberichi Eze, baada ya kuzidisha dau lililowasilishwa kuchelewa na West Brom kumpata mchezaji huyo aliye na umri wa miaka 22- Fulham walijiondoa.
Tetesi zinasema Aston Villa, Leeds United na West brom pia wanamsaka Watkins.
Everton, Leicester City, Southampton na Leeds United wamewatuma wasaka vipaji wao kufuatilia mchezo wa kiungo wa safu ya kati na nyuma wa Dundee United Lewis Neilson, 17.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.
Ester jackson
Barcelona sasa inaelekea pabaya mana wachezaji wenye uwezo wa kuifikisha timu mbali wanataka kuondoka inakuwa hatari sana
rama
daaa itakuwa vizuri sana abadilishe mazingira
Mwajumah
Sio mbaya atakuwa anabadilisha mazingira#Meridianbettz
Mwanahamisi
Bora aende akaangalie upepo mwingine
Khadija
Habari njema
Sylvester
Messi na Philippe Coutinho ni wachezaji bora ambao itakua vizuri Philippe Coutinho kurudi tena kwenye viunga vya Uingereza wakati Messi nae aje kuonyesha cheche zake pale Uingereza ili kunogesha kidogo EPL
Fatina mfigi
Ni Jambo zuri m2 kutoka sehemu moja kwenda nyingine
Zeiyana
Barcelona wana halingumu sana hadi kukamilisha kikosi chao kuna kazi ya ziada
Caroline
Sidhani Kama Messi ataondoka Barcelona
Sauda
Ni bora akabadilishe upepo
Tatu
Man wanamutaji sana messi ila sijui kama mwenyewwe atakubali kiacha barcelona
felister
Bora akabadili mazingira mana amekaa sana barcelona
Dorophina
Messi ni bora haende man u itakuwa poa sana
Rehema
Hii ni habari njema
Adelta
Mashabiki tunashukuru kwa taarifa
@meridianbettz
Fatuma kasomo
Aende abadili upepo
aisha
Messi hawezi kuondoka barcelona maana akiondoka itakuaje
Salma ngende
Habari njema
Issa
Chelsea imepata beki wa viwango vyake
Neema
Naona ni sawa tu akabadili mazingira
Leonard
Itakuwa habari nzuri kama messi ataondoka
Sadick
Thiago Silva ni beki kiongozi ingawa umri wake mkubwa#meridianbettz
farida ahmadi
Habari njema Sana
Shan
Zimekaa vizuri sana.
Latifa juma mohamed
Sasa kwa Barca itakuwa hatar I km wachezaji wazur wakisepa timi itaxid kulega.
Saupha mohamed
Good news
Hope mwaikuka
Popote kambi mrad mkono uende kinywan
Gabriel
Waswahil tunasema adui wako muombee njaa atakuheshim tu ata Kama alikuwa shujaa upande wang nimejifunza hilo maana usajil wa Messi kwenda PSG kutawafanya wakae vzur pia inatakiwa ndo wakae wajipange vzur Barcelona kwa hilo
Rose kapinga
Messi ni wa Barcelona tu!!
Povel
Nice update
Sabrina
Messi atasepa tu barca
Amiri Kayera
Apo vilabu wajimaliz kushawish
Shafii
Hizi zimekaa poa.
Lydia Emmanuel Magoti
Duu Barcelona kimenuka Hari yahewa imetibuka Sasa mwisho wabarcelona nikushuka kimpila nawatu wakiondoka itabaki Barcelona jina sasa
Ernest
Messi kaipiga pigo kubwa sana Barcelona maana pengo lake bado hawakutafuta mbadala
Furahav
Habari njema.
David Pere
Messi na Philippe Coutinho ni wachezaji bora ambao itakua vizuri Philippe Coutinho kurudi tena kwenye viunga vya Uingereza wakati Messi nae aje kuonyesha cheche zake pale Uingereza ili kunogesha kidogo EPL
magdalena
messi na coutinho ingependeza sana wangekuja united #meridianbet
warda
Messi nae atupe break kidogo
Samiah
Nice
Devotha
Hizi bado ni tetesi tu