Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa Everton na England Dominic Calvert-Lewin, 25, anatarajia kuondoka kwenye klabu hiyo mwishoni mwa msimu, huku Arsenal na Newcastle United zikonyesha nia ya kumtaka.

Tetesi zinasema, Real Madrid wanaripotiwa kumtaka kiungo wa Manchester City na Ujerumani Ilkay Gundogan, 31.

Newcastle United hawatamsajili kiungo anayemaliza mkataba Manchester United Jesse Lingard, vinginevyo kama atapunguza mshahara anaotaka wa £150,000 kwa wiki.

 

Jesse Lingard.

Tetesi zinasema, Mlinzi wa Barcelona na Ufaransa Samuel Umtiti, 28, anaweza kutua Arsenal kwa mkopo.

Tetesi iznasema, Liverpool wanajiandaa kusikiliza ofa kwa ajili ya kiungo wake wa England Alex Oxlade-Chamberlain, 28, msimu huu.

Barcelona wanajiandaa kumuuza mlinzi wa kati wa kimataifa wa Hispania Oscar Mingueza, 23 msimu huu huku wakali hao La Liga wakitaka angalau £4.2m ili kumuachia.

Tetesi zinasema, Kiungo wa Ufaransa Paul Pogba, 29, atajiunga na Paris St-Germain au Juventus atakapoondoka Manchester United bure msimu huu.

 

Pogba

Manchester United itasikiliza ofa kwa ajili ya beki wake wa kushoto muingereza Brandon Williams, 21 msimu huu baada ya kuitumikia Norwich City kwa mkopo msimu huu.

Kiungo wa Ujerumani Pascal Gross, 30, na mshambuliaji wa England Danny Welbeck, 31, wanakaribia kusaini mikataba mipya Brighton.

Mlinzi wa pembeni wa Wolves na Ureno Nelson Semedo, 28, anatarajia kusalia klabuni hapo kwa muda mrefu zaidi licha ya sasa kutokuwepo kwa mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe