Tetesi zinaasema Manchester United wiki ijayo itaweka mezani dau la mwisho la £90m kwa ajili ya kujaribu kumsajili winga wa England Jadon Sancho, 20, kutoka Borussia Dortmund.
Tetesi zinasema Arsenal wameonyesha nia ya kumsajili kiungo wa Chelsea na Italia Jorginho, 28.
Lucas Torreira anakaribia kuondoka Arsenal, huku klabu za Atletico Madrid na Torino zikionyesha nia ya kumnasa kiungo huyo wa Uruguay, 24.
Atletico Madrid wanaamini watamnasa Torreira kwa mkopo, hatua itakayoifanya Arsenal nayo kumsajili kiungo wa timu hiyo ya Hispania Thomas Partey, 27, raia wa Ghana.
Manchester City imesema madai kwamba imeweka ofa ya £78m kwa ajili ya mlinzi wa Atletico Madrid na Uruguay Jose Gimenez, 25, sio kweli.
Tetesi zinasema Monaco imeonyesha nia ya kumsajili kiungo wa Tottenham na England Dele Alli, 24,
Paris St-Germain wanatarajia kujiondoa kwenye mazungumzo ya kumsajili Alli kwa mkopo wa muda mrefu.
Mshambuliaji wa Chelsea na England Callum Hudson-Odoi, 19, anataka kuondoka Stamford Bridge kwa mkopo .
Kiungo mchezeshaji wa Barcelona na Brazil Philippe Coutinho, 28, anaweza kwenda kwa mkopo Arsenal kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
RB Leipzig wanakaribia kumsajili mlinzi wa kati, hatua itakayosaidia mlinzi wake Dayot Upamecano kuondoka klabuni hapo. Manchester United imekuwa ikihusishwa kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21.
Mshambuliaji wa Napoli Arkadiusz Milik amewekwa sokoni kwa kikosi cha Everton cha Meneja Carlo Ancelotti, lakini Muitaliano huyo akiwa na joto la kutaka kuungana nae tena nyota huyo wa kimataifa wa Poland, 26.
Sheffield United inaongoza mbio za kumsajili mshambuliaji wa Liverpool , Muingereza Rhian Brewster, 20, huku klabu za Aston Villa, Brighton na Crystal Palace zikionyesha nia ya kumsajili.
West Ham na Aston Villa ni miongoni mwa vilabu vinavyomtaka kumsajili kiungo wa Chelsea na England Ruben Loftus-Cheek, 24, kwa mkopo wa msimu mzima.
Southampton wanatarajia pia kukamilisha usajili wa kiungo wa Toulouse na Ivory Coast Ibrahim Sangare, 22.
Tetesi zinasema Everton na Fulham wanamuania mlinzi wa Cameroon Jerome Onguene, 23, kutoka RB Salzburg.
West Brom wanaweza kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Manchester City Emmanuel Adebayor, 36, kama watashindwa kumnasa mshambuliaji mwingine kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Mlinzi wa St Etienne Wesley Fofana anaweza kutua Leicester City lakini mpango wowote utakaokubaliwa utakaomfanya kinda huyo wa umri wa miaka 19 asalie kwenye Klabu hiyo ya Ufaransa.
Tetesi zinasema Meneja wa Southampton Ralph Hasenhuttl anataka kusajili wachezaji watatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Bayern Munich hawatamruhusu kiungo wa Ufaransa Michael Cuisance kuondoka kwa mkopo, licha ya Leeds United na Marseille kuripotiwa kuonyesha nia ya kumsajili nyota huyo wa umri wa miaka 21.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.
magdalena
united hawataki kukata tamaa kabisa juu ya kumsajili sancho
Adelta
Manchester united wafanye juhudi ili waweze kumchukuwa Sancho
Gabriel
Arsenal wameonyesha nia ya kumsajili Jorginho imekaa poa sana kuelekea kukiandaa kikosi kuwa kizur zaid
Samiah
Gud
Mwajumah
United naona bado wanampambania sancho hawataki kabisa kukata tamaa juu ya kumsajili
Frank P
Koeman kashasema coutinho yupo kwenye mipango yake
Zeiyana
Man Chester united wanapigania sana sain ya sancho
Sauda
Man U fanyeni mpango mchukue jembe hilo.
Elika
Safi sana man
Sadick
Man U haijakata tamaa kumutaka Jadon Sancho#meridianbettz
Shan
Inabidi ifike mahali wakubaliane
Dorophina
Man u inabidi wasikate tamaa kwenye usajili wa sancho lazima aje man u
Nasra
Nice 👍
Lydia Emmanuel Magoti
Man U fanyeni mpango kiereweke
Khadija
Safi sana man
Caroline
Asante kwa taarifa
Tatu
Usajili umepamba moto kila mtu anajiandaa ipasavyo
Janeflora malisa
Good
Fatuma kasomo
Safi
Rose kapinga
Ongezeni dau mambo yasiwe mengi,kizuri gharama!!!
Issa
United waache maneno wamchukue sancho
Hopemwaikuka
Zko vzur sana
Rehema
Gud news 👍
Tumaini kasalile
Man utd kazeni buti mumpate sancho
aisha
Man u wamchukue sancho wasilet maneno
Sabrina
Man u hawakati tamaa
felister
ahsante kwa taarifa
Amiri Kayera
Duh ili Dau la Sancho pasua kichwa
David Pere
Arsenal wameonyesha nia ya kumsajili Jorginho imekaa poa sana kuelekea kukiandaa kikosi kuwa kizur zaid