Tetesi zinasema Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta amesema kuwa amempatia mchezaji nyota wa zamani wa klabu hiyo Mesut Ozil ,32, “nafasi nyingi” kadri ya uwezo wake kabla ya kumuacha nje ya kikosi cha Ligi ya Primia na Ligi ya Europa.
Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola, ambaye kandarasi yake katika klabu hiyo inamalizika msimu ujao amepuuzilia mbali tetesi zinazomhusisha na kurejea Barcelona.
Tetesi zinasema Barcelona inatarajiwa kurejelea tena jitihada za kumsajili mlinzi wa miaka 19 wa Manchester City Eric Garcia mwezi Januari dirisha la uhamisho litakapofunguliwa.
Carlo Ancelotti anasisitiza kuwa mshambuliaji Moise Kean,20 atarejea msimu ujao kujiunga na Everton mkataba wake wa mkopo Paris St-Germain utakapokamilika.
Mkufunzi wa Bayern Munich Hansi Flick ana matumaini kuwa mlinzi wake David Alaba, 28, raia wa Austria atakubali kutia saini kandarasi mpya ya kusalia katika klabu hiyo.
Kocha wa England Gareth Southgate anajiandaa kumjumuisha beki wa kulia na nyuma wa Manchester Luke Shaw, 25, katika kikosi cha kimataifa, baada ya kumteua tangu mwezi Machi mwaka 2019.
Nyota wa Wales na Spurs Gareth Bale ametoa msaada wa £15,000 kufadhili zawadi 300 za Krismasi zitakazopewa watoto walio na uhitaji zaidi Wales.
Tetesi zinasema Mkurugenzi wa soka wa Arsenal Huss Fahmy anatarajiwa kuondoka klabu baada ya kujiunga na Gunners miaka mitatiu iliyopita.
Wakala wa ngazi ya juu Mino Raiola amewasili AC Milan kuanza mazungumzo ya kurefusha mkataba wa kipa Gianluigi Donnarumma, 21, na mlinzi Alessio Romagnoli, 25.
Tetesi zinasema Atletico Madrid wanajiandaa kumsajili kiungo wa kati wa Valencia na Jamhuri ya Afrika ya Kati Geoffrey Kondogbia, 27.
Derby County inakaribia kununuliwa na Sheikh Khaled bin Zayed Al Nehayan of Abu Dhabi, ndugu wa mmiliki wa Manchester City Sheikh Mansour.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
Adelta
Ziko vizuri na zinasomeka
Ester Jackson
Sasa matunda mema kwa bale yanaonekana hongera sana
Sauda
Barcelona wakimpata Eric Garcia watakuwa wamelamba dume.
Fatina mfingi
Hongerin arsenal kwa kupata jembe!
Ernest
Bale katisha
zeiyana
ongera sana bale
Khadija
Bale yupo vzr
Angelina
Good job bale
Lydia Emmanuel Magoti
Safii Sana bale
Nasra
Safi sana
Sabrina
Bale yuko fiti
Mwajumah
Hongera sana Bale
Carolyn
Asante kwa taarifa
Elika
Bale Yuko vizurii
Tatu
Barcelona wameamua kuongeza wachezaji
Hopemwaikuka
Sio mbaya
julieth
safi sana
Issa
Ozil tafuta chaka
Povel
Nice update
Fatuma kasomo
Safi
aisha
Bale yuko vizuri sana
Saupha mohamed
Ozil yupo vizuri
warda
Habari poa sana
Salma ngende
Safi sana