Kocha mpya wa Chelsea, Thomas Tuchel, anatarajia kuwaleta watu wake anaowaamini katika benchi lake la ufundi.
Tuchel amekabidhiwa mikoba ya Frank Lampard ambaye alioneshwa mlango wa kutokea Stamford Bridge baada ya kuiongoza timu hiyo kwa miezi 18. Kibarua cha kwanza kwa Tuchel kilikuwa ni mchezo dhidi ya Wolves ambapo walimaliza kwa sare ya 0-0.
Imeripotiwa kuwa, Thomas Tuchel anatarajia kumleta Arno Michels ambaye atakuwa ni msaidizi wake na Zsolt Low pia ataungana nae kwenye benchi lake la ufundi katika klabu ya Chelsea.
Chelsea itatoatamko rasmi kuhusu uteuzi wa benchi jipya la ufundi ambapo, Michels amekuwa msaidizi wa Tuchel tangu alipokuwa Borussia Dortmund na hata PSG. Pia, Tuchel alivutiwa na uwezo wa Low alipokutana naye PSG na anatarajia kuendelea kufanya nae kazi katika EPL.
Imeripotiwa kuwa, Tuchel ni mtu anayependa kufanya kazi na watu anaowaamini. Hii ni sababu kubwa inayomfanya aambatane na benchi lake la ufundi kwenye kila timu aliyoifundisha mpaka sasa.
Licha ya Chelsea kumtimua Lampard, klabu hiyo imeadhimia kuwabakiza baadhi ya watu waliokuwa wakifanya nae kazi, hii ikiwa ni pamoja na Joe Edwards, Anthony Barry, Henrique Hilario, Matt Birnie na Will Tullett ambapo hawa wote walionekana wakisaidiana na Thomas Tuchel kwenye uwanja wa mazoezi kuelekea mchezo dhidi ya Wolves.
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri
Magdalena
Safi Sana kazi nzuri
Adelta
Kazi nzuri 👏👏
samiah
Vzr
Dorophina
Tunasubilia kuona chelsea ikiinuliwa na tuchel
Caroline
Safiiiii sana
Venerose
Inapendeza
Mwanahamisi
Vizuri
Ernest Kimeru
Tuchel anamzigo mkubwa sana kubadilisha hali iliyopo sasahivi Darajani
Issa
Tuchel imeingia kwenye kaa la moto
Sania
Tuchel kazi anayo
Hopemwaikuka
Shughuli ipo