Toni Kroos: “Real Madrid Ndiyo Timu Hatari Zaidi Duniani Mambo Yanapokuwa Hayaeleweki"

Nyota wa Ujerumani Toni Kroos ameweka wazi wakati muhimu zaidi katika mchezo wa Real Madrid dhidi ya Bayern Munich.

Toni Kroos: “Real Madrid Ndiyo Timu Hatari Zaidi Duniani Mambo Yanapokuwa Hayaeleweki"

Gwiji wa Ujerumani Toni Kroos, ambaye ni mmoja wa waliowahi kuwa nguzo ya Real Madrid, aliuchambua ushindi wa Bayern Munich wa mabao 2-1 dhidi ya Los Blancos katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Akizungumza kwenye podikasti yake, Kroos alisema: “Sikushangazwa na kilichotokea kwenye mchezo huo. Ingawa Bayern walicheza vizuri sana, kilichotokea baada ya kuwa wanaongoza 2-0 ndiyo kilikuwa cha kuvutia zaidi kutoka upande wa kisaikolojia.”

“Katika miaka ya hivi karibuni, Bayern wamekuwa wakiwadhibiti Real Madrid katika mchezo wa kwanza, lakini mara nyingi hushindwa kudumisha kiwango hicho au kufuzu kwenye mchezo wa marudiano mambo madogo madogo huishia kuwagharimu.”

Uongozi wa 2–0 wakati wa mapumziko ulipaswa kiakili kuufunga mchezo. Badala yake, Bayern Munich walirudi nyuma na kucheza kwa intensity ndogo zaidi katika ulinzi. Alisema Kroos.

Toni Kroos: “Real Madrid Ndiyo Timu Hatari Zaidi Duniani Mambo Yanapokuwa Hayaeleweki"

Wakati huo Bayern walikuwa na udhibiti kamili wa mchezo, hivyo alitarajia waendelee kudumisha ubora wao au kuongeza bao la tatu. Nilitegemea wangeshikilia mpira kwa utulivu au kuongeza bao la tatu, la nne, hata la tano; lakini kinyume chake ndicho kilichotokea.

“Kosa lililofanywa dhidi ya Vinícius Júnior lilikuwa turning point ya mchezo. Baada ya hapo, Real Madrid walionyesha nguvu ya tabia yao na kutengeneza nafasi kadhaa hatari kati ya dakika ya 60 hadi 75 licha ya kuwa nyuma 0–2.”

Gwiji huyo amesema kuwa kwa maoni yake, Real Madrid ndiyo timu hatari zaidi duniani pale mechi inapogeuka kuwa ya kushambuliana ovyo (attacking free-for-all)… Huu ni mtindo wanaoupenda sana.

Alimalizia: “Ndiyo maana Real Madrid walikaribia kusawazisha; mchezo ungeweza kuisha 3–3, lakini uliisha 2–1. Kwa mtazamo wangu, Bayern Munich walipaswa kuudhibiti mchezo vizuri zaidi ama kulinda uongozi wao au kutumia nafasi zao kuongeza mabao hadi 3–1 au 4–1.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.