Kwa mujibu wa Caught Offside, Tottenham wanajiandaa kuwasilisha ofa ya kumsajili mshambuliaji wa Liverpool, Cody Gakpo, huku kukiwa na mashaka kuhusu mustakabali wake ndani ya klabu hiyo.

Tottenham Spurs walinusurika kushuka daraja kwa taabu msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Uingereza na wanahitaji kuhakikisha hali hiyo haijirudii. Tayari wameimarisha safu yao ya ulinzi kwa kumsajili Marcos Senesi kutoka Bournemouth, na sasa wanaelekeza nguvu zao katika kuimarisha safu ya ushambuliaji.
Ripoti za awali zilidai kuwa Tottenham wanamtaka Gakpo, na sasa Caught Offside imethibitisha madai hayo, ikieleza kuwa klabu hiyo ya kaskazini mwa London inajiandaa kuwasilisha ofa kubwa kwa nyota huyo wa Uholanzi.
Baada ya kushuka kiwango msimu uliopita, mustakabali wa Gakpo ndani ya Liverpool umeingia kwenye sintofahamu, na Tottenham wanaonekana kuwa na hamu ya kutumia hali hiyo kwa manufaa yao.
Inaelezwa kuwa Tottenham Spurs ndio wanaoongoza katika mbio za kuwania saini ya Gakpo na wana mpango wa kutoa euro milioni 70 (sawa na pauni milioni 60.4) kwa ajili ya huduma zake.




