Imeripotiwa kuwa ni wazi, Kieran Trippier anataka kuondoka Atletico Madrid na kurejea Uingereza msimu ujao.
Manchester United wanamtizama Trippier kama mtu sahihi wa kumpachangamoto Aaron Wan Bissaka kutokana na uzoefu na namna ya uchezaji wake (kukaba na kushambulia).
Tayari United wameshatolewa nje na Atletico kwa dau la kwanza walilotoa ili kumsajili Kieran. Kukosa kwa dau la kwanza, hakuwaotoi United mchezoni. Wanauwezo wa kurudi na dau kubwa zaidi.
Zikiwa zimesalia wiki 4 tu kuelekea msimu ujao wa EPL, Kieran anaadhimia kurejea kwenye EPL na inasemekana sio United tu wanaomnyatia, kuna timu zingine 2 za EPL zinamtazama beki huyo kwa jicho la kipekee na hivyo lolote linaweza kutokea kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!
dorophina
Man u mbona kama wamepania sana usajili wa msimu huu