Tsitsipas Bingwa wa Monte Carlo Masters.

 

Mcheza Tenisi wa Ugiriki, Stefanos Tsitsipas amefanikiwa kutetea taji lake la Monte Carlo Masters kwa ushindi wa moja kwa moja dhidi ya Alejandro Davidovich Fokina hapo jana alilokuwa akilishikilia tangu mwaka jana.

Tsitsipas alimfunga Davidovich Fokina ambaye amewashangaza wengi baada ya kuwaondoa Novak Djokovic na bingwa wa Indian Wells Taylor Fritz katika raundi za awali.

 

 

Tsitsipas alikosa nafasi kadhaa kwenye mechi hiyo katika seti ya pili lakini alijipanga upya na kutwaa ushindi wa 6-3 7-6 (7-3) ndani ya dakika 90, huku ushindi huo ukitarajiwa kumfanya asogee hadi nafasi ya pili katika mbio za ATP hadi Turin.

“Ninajivunia sana,” Tsitsipas, 23 alisema kwenye tovuti ya ATP.

“Mambo hayakuwa sawa kwa wakati mmoja, lakini nilifanikiwa kukaa sawa ili kumaliza mechi, najivunia imani niliyoiweka kwenye mchezo wangu. Wakati mwingine unajitilia shaka, lakini ni muhimu kuinua kichwa chako juu.”


VUNA MKWANJA NA AVIATOR

Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI

Acha ujumbe