Guardiola: Hatujali Kabisa!

Kocha wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola alisema kwamba hatojali lolote lile endapo kikosi chake kingemaliza msimu bila kuwa na taji lolote. Kocha huyo ametasema hayo kwa kuona kwamba hana wasiwasi wa namna ambavyo wengi wanahisi hatakuwa na amani kunyanyua kikombe ndani ya msimu huu kutokana na kuwa na matokeo mabovu ambayo hayaendani kabisa na kasi yake ya msimu uliopita.

Kocha huyo aliona kwamba hadi sasa mataji ambayo aneyanyanyua mfukulizo na klabu hiyo ni kipomo tosha kabisa cha kuweza kuaminisha kwamba anaweza kazi yake hiyo. Amenyanyua kombe la ligi mara mbili mfululizo akiwa na kikosi hicho na makombe mengine ya ndani. Kwa hiyo suala hilo halimpi wasiwasi.

Ramani hiyo imeanza kuonekana mara baada ya kocha huyo kuona kwamba watu wameanza kumwangalia kwa namna nyingine kutokana na kupoteza mechi yake mbele ya klabu iliyopanda ligi msimu huu pia mara baada ya kuwa na mwenendo ambao kikosi chake kinaonesha kusuasua sana ndani ya ligi hiyo.

Maajabu ambayo hayatasahaulika kwa kocha huyo ni kunyanyua kombe akiwa na alama nyingi sana katika ligi ambazo zilikuwa 98 jambo ambalo kwa miaka ya karibu lilikuwa kama historia na mapinduzi makubwa katika soka la Uingereza. Hivyo, kwake hilo sio changamoto na aliliona halina nguvu kumpa mawazo sana.

Jimgine ambalo kocha huyo alijaribu kulizungumzia ni juu ya hali halisi ilivyo kikosini hapo kwa sasa kwamba sio rahisi sana kutokana na kuanza msimu kwa kuwa na wachezaji ambao ni majeruhi, tena wachezaji ambao ni muhimu sana katika kikosi chake cha kwanza; hivyo hilo ni jambo ambalo kwake bado ni changamoto kiasi fulani.

Akiwa kama kocha pia amezungumzia suala la kuwa na wach3zaji wa aina moja katika misimu kadhaa mfululizo kwamba nalo huwa linashusha ushindani kwa sababu kikosi hicho huwa tayari kimeshinda kila kitu na kuona kwamba ni hali ya kwaida sana hata pale wanapotokea kukosa ubingwa fulani.

Lakini mbali na hilo ametahadharisha kwamba hilo sio sababu ya yeye kukata gamaa ya kufukuzia ubingwa bali ni onyo tu la kawaida ambalo ameliweka kwa wale wanaoona kwamba kocha huyo huenda ameanza kukubali hali halisi ya ligi kwa msimu huu. Kwamba atashindwa kufanya vyema kabisa.

40 Komentara

    man saiv amna kitu wabovu

    Jibu

    Kocha wa Manchester city
    Anajitahidi Sana japokuwa anipitia
    Changamoto

    Jibu

    Man u wameshaishiwa

    Jibu

    Ni ulemsemo wa sizitaki mbichi hizo Pep anautumia apo

    Jibu

    Kwa uwekezaji mkubwa kama wacity alafu kumaliza msimu bila kombe lolote!!!

    Jibu

    Pep ni jasiri sana

    Jibu

    Pep ni kocha bora

    Jibu

    kashaishiwa uyo Hana lolote

    Jibu

    Anajibaraguza huyo

    Jibu

    Huyu ni aina ya makocha wanaojua nini wanafanya …

    Jibu

    Anajipa moyo tu,uku kiroho kinauma

    Jibu

    Anatakiwa asifanye ivo ,apambane ili wafikie malengo.

    Jibu

    hiyo ni kocha anayejua#meridianbettz

    Jibu

    Guardiola yuko vizuri anajikubali sana na ndio maana hajali chochote kile

    Jibu

    Hana jipya anajishitukia tu huyo anarapu tu hapo ila moyoni kunaongea vingine

    Jibu

    Kila mtu anamapungufu yake ila Guardiaola aliweza fanya Mambo mazuri tu

    Jibu

    Pep bado ni kocha bora kwa upande wangu

    Jibu

    Shuhul mnayo watu wa man

    Jibu

    Pepe kwa upande wake yuko sahihi kabisa ila mashabiki watahitaji waone man city inachukua taji

    Jibu

    Big coach pep namkubali Sana! Safari hii Liverpool anastahili tumpe ubingwa wake.#meridianbettz

    Jibu

    Kocha pep Guadiola ni kocha anayejiamini anaamini yeye si mtu wa kushindwa hii iko poa sana

    Jibu

    Guadiola ni kocha mwenye upeo mkubwa anajua n Nini anafanya

    Jibu

    Guardiola unazingua maneno gan ayo ya kutatsha tamaa wachezaj na mashabiki

    Jibu

    Man hawana jipya..

    Jibu

    hilo sio sababu ya yeye kukata tamaa ya kufukuzia ubingwa #meridianbettz

    Jibu

    tena wachezaji ambao ni muhimu sana katika kikosi chake cha kwanza; hivyo hilo ni jambo ambalo kwake bado ni changamoto kiasi fulani. #meridianbet

    Jibu

    Pep ni moja Kati ya makocha Bora dunia kwa Sasa thnks meridian kwa update za michezo

    Jibu

    Pep ni jasiri sana napia ni kocha nzur sana

    Jibu

    Pep bado Yuko vzr

    Jibu

    Ashawachoka sana

    Jibu

    Mbinu zishaisha Hana Tena ujanja inabidi akubali matoke

    Jibu

    Hatutaki maneno si tunataka vitendo mashabiki

    Jibu

    Gadiola sijaipenda maneno yako

    Jibu

    huyu pep anajifariji tu anyway mwache ajidanganye maboss zake ni watu wa maamuzi ya haraka

    Jibu

    Pep yupo vizuri

    Jibu

    Man ilikuwa zamani bhanaa

    Jibu

    Gadiola uwenda kunaacho jivunia

    Jibu

    Ni kocha mzuri Sana na anatambua anachokifanya

    Jibu

    Pep ni kocha bora

    Jibu

    Guardiola ni kocha mahiri asiyenamfanoe kwa sasa hapa duniani #meridianbettz

    Jibu

Acha ujumbe