Mwanamasumbwi wa Uzito wa juu Tyson Fury kwa mara nyingine amedai kuwa ataachana na mchezo huo baada ya pambano lake na Dillian Whyte ambalo linatarajiwa kuchezwa wikiendi hii.
Fury mwenye miaka 33 anatarajia kuweka rehani mkanda wake wa uzito wa juu wa WBC ulingoni siku ya jumamosi kwenye uwanja wa Wembley dhidi ya mpinzani wake Whyte mwenye miaka 34.

Fury amekubali kuwa hili ndio pambano lake kubwa nyumabani na litakiwa la mwisho kwenye maisha yake ya mafanikoya mchezo wa ngumi, lakini ameapa atafanya kadri awezavyo kuweza kushinda.
“Sina cha kuthibitisha kwe yeyote, nipo kwa ajiri ya kufurahi, kuweka hali ya hewa sawa na kufurahia usiku wa pambano. ndio kwaheri ya mwisho, ilikuwa ni safari ndefu, ni hisia kali kuwa mkweli.
“yote haya, ni kama safari, anayoanza mtoto mdogo na yakutaka kuwa bingwa wa uzito wa juu, na kisha mishowe anatundiga glavu.
‘Najua hakuna anayeniamini kwa sababu wanadhani nipo kwa ajiri ya pesa au vyovyote vilem kuna watu wachache ambao wanajua kwamba pesa haina maana kwangu.
‘Naachana nao. Sina cha kuthibitisha kwa mtu yeyote. Nimemaliza nilichotakiwa kufanya. Kushinda, kupoteza au kutoa droo siku ya jumamosi, tutakuwa na pambano zuri na kurudi nyumbani hivyo.” Alisema Tyson Fury.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.