Uingereza wanatarajia kuwakabili timu ya taifa ya Italia kwenye dimba la Molineux wolves siku ya jumamosi kwenye mchezo wa UEFA Nations League pasipo mashabiki kutokana na vurugu walizofanya kwenye mchezo wa fainali ya Euro 2020.
Uingereza anakutana na italia kwa mara ya kwanza tangu mchezo wao wa mwisho wa fainali ya Euro 2020 ambapo Italia alifanikiwa kushinda kwa mikwaju ya penati, Mchezo wa leo unatarajiwa kuudhuliwa na wanafunzi 3000 tu wakiwa na umri wa chini ya miaka 14 na kwa sheria za UEFA watatakiwa kuingia bure.
Pia kutokana vurugu zilizofanywa na mashabiki wa Uingereza kwa furaha zao za kushiriki fainali ya kwanza tokea mwaka 1966, chama cha soka FA kilipigwa faini ya £84,560 kutokana na mataukio hayo ya vurugu za mashabiki wake.
Kocha wa timu ya taifa Uingereza Gareth Southgate alilaani vitendo hivyo vilivyofanya na mshabiki na kunukuliwa akisema, “kama ni aibu, ni Uingereza kama nchi ndio imeaibika, watu wengi waliosababisha vurugu sina hakika kama ni mashabiki wa mpra.
“Tulizungumza kuhusu hili vya kutosha, Tulizungumza kuhusu hili baada ya mchezo wa fainali na tulipo pewa adahabu kwa mara ya kwanza.”
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.