Ukweli Kuhusu Cristiano Ronaldo Kusajili Saudi Arabia

Cristiano Ronaldo atasaini mkataba wa £175m kwa mwaka na klabu ya Saudi Arabia Al Nassr kabla ya mwisho wa mwaka, kulingana na jarida Marca.

Mkataba wa Ronaldo mwenye umri wa miaka 37 katika Manchester United ulikatizwa mapema mwezi huu baada ya kuiangazia klabu katika mahojiano na Piers Morgan.

 

ronaldo

Ronaldo ambaye kwa sasa yuko Dubai, alihusishwa na klabu hiyo ya Saudi Arabia kabla ya Kombe la Dunia la 2022 nchini Qatar lakini alikataa kutoa maoni yake kwa kuwa alikuwa anaangazia zaidi dimba hilo.

Kulingana na Marca, Al Nassr wanataka kumsajili Ronaldo kabla ya mwisho wa mwaka na wamempa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 mkataba mnono wa £175m-kwa mwaka ili kupata huduma yake.

Ronaldo na familia yake inasemekana wako Dubai hadi mkataba huo utakapokamilika ambapo, unajumuisha makubaliano ya utangazaji uthibitishwe.

 

ronaldo

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno alikataa kuhamia Saudia msimu uliopita wa joto, lakini bila maslahi yoyote madhubuti kutoka kwa vilabu bora vya Ulaya, anaelekea sasa kuhama.

Al Nassr ni moja ya vilabu vilivyofanikiwa zaidi nchini Saudi Arabia, baada ya kutawazwa washindi wa ligi kuu ya nchi hiyo mara tisa, na ushindi wao wa hivi karibuni unakuja mnamo 2019.

Mnamo 2020 na 2021, Al-Nassr wanaweza kuwa hawajashinda ligi, lakini walifanikiwa kushinda Kombe la Super Cup la Saudi. Hata hivyo, wametatizika kujitokeza katika ulimwengu. Mchezo wao pekee wa Kombe la Dunia la Vilabu ulikuja msimu wa 1999-2000, ambapo walicheza dhidi ya moja ya vilabu vya zamani vya Ronaldo, Real Madrid, na kufungwa 3-1.

 

ronaldo

Waliendelea kuifunga Raja Casablanca 4-3 lakini wakafungwa 2-0 na Corinthians ya Brazil huku wakikosa nafasi ya kufuzu kwa shindano hilo.

Al Nassr kwa sasa inanolewa na Mfaransa Rudi Garcia, ambaye amewahi kuzifundisha Roma, Marseille, na Lyon. Pia hucheza katika uwanja wenye uwezo wa kubeba mashabiki  25,000.

Ronaldo kujiunga na Al Nassr itakuwa kumbukumbu kwa klabu na nchi kwa ujumla kutokana na kwamba wanatazamia kuwa taifa kubwa la kimichezo.

Waziri wa Michezo wa Saudi Arabia hapo awali alidai ‘angependa’ kumuona Ronaldo akicheza katika ligi ya taifa hilo.

Akizungumza na BBC Sport, Mwanamfalme Abdulaziz alisema: ‘Lolote linawezekana, ningependa kuona Ronaldo akicheza kwenye ligi ya Saudia.

‘Itafaidi ligi, mfumo wa ikolojia wa michezo nchini Saudi na itawatia moyo vijana kwa siku zijazo. Yeye ni mfano wa kuigwa kwa watoto wengi na ana msingi mkubwa wa mashabiki.’

Uhamisho wa Ronaldo kwenda Al Nassar unakuja muda mfupi baada ya mkataba wake na wababe wa Ligi Kuu, Manchester United, kuvunjwa.


Bashiri na kitochi au bila bando mechi hii, Bonyeza hapa kutazama ODDS kubwa na bomba kupitia machaguo spesho ya meridianbet ili kuingia mchezoni. Pia ukibashiri na kitochi kwa dau la TZS 1,000/= Unaweza kuibuka mshindi wa MBUZI WA KITOWEO CHA SIKUKUU, kila wiki Ijumaa.

Acha ujumbe