Tukiwa tunahesabu siku chache kabla ya dirisha dogo la usajili kufunguliwa Januari 1, 2021. Fununu zinaendelea kushika kasi!!!
Fununu za usajili zinasema Arsenal wanapanga kumpeleka Mesut Ozil Juventus kwa mkataba wa miezi 6 huku wakilipa sehemu kubwa ya mshahara wake. Ikumbukwe, Ozil amebakiza mkataba wa miezi 6 kuendelea kuwepo Emirate na alishagoma kuondoka mpaka mkataba wake uishe.

Arsenal watafanikiwa katika hili??

Arsenal haohao wanaimani watawazidi kete Man City na Bayern Munich kwa kinda anayekuja kwa kasi – Tariq Lamptey anayekipiga katika klabu ya Brighton, Arteta anamuona Lamptey kama mtu sahihi wa kuziba pengo la Bellerin kama beki huyo ataamua kurudi Barcelona.

Hali sio shwari kule Etihad, za chini ya kapeti kwenye usajili zinasema Phil Foden hafurahishwi na nafasi finyu anayoipata kwenye kikosi cha Pep Guardiola msimu huu. Ikumbukwe matanio ya Foden ni kupata nafasi kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Uingereza kwenye mashindano ya Uero mwakani.

Unaambiwa mcheza kwao hutuzwa, Tottenham kumrudisha Christian Eriksen mwezi Januari ikiwa ni mwaka mmoja tangu atimkie Inter Millan. Endapo usajili huu utafanikiwa, utakuwa na maana yeyote kwa Eriksen na Tottenham??

David Moyes anaamini Declan Rice anaweza kubakizwa West Ham, Moyes anaamini njia pekee ya kuwaondoa Chelsea kwenye ramani ni kumuongezea mkataba mnono Rice.

The Red Devils – Manchester United wamejiondoa kwenye kinyang’anyiro cha kumuwania David Alaba. Fununu zinasema United wanazingatia zaidi mtonyo mrefu ambao beki huyo atauhitaji ili atue Old Trafford.

Za kunyapianyapia zinatuambia, PSG wamemaliza mchongo wa kumkabidhi Mauricio Pochettino kikosi cha timu hiyo, hii ni baada ya kukamilisha utaratibu wa kumlipa fidia Thomas Tuchel ambaye anatajwa kupokea kitita cha pauni milioni 5.4.
Tuambie unatamani kuona usajili wa mchezaji gani ukifanyika 2021???
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Adelta
Ngoja tusubiri usajili wa Arsenal kama utafanikiwa!
Sarah
Tunasubiri usajili tuone itakavyokuwa
Chiku
Tunawangoja kwa hamu
Shakila mrope
Yetu macho tusubilie tuone
Tatu
Ngoja tuone nani atalamba galasa nani atalamba dume
Mwanahamisi
Ngoja tuone
Dorophina
Tunasubilia usajili tu nan atabaki na nan atasepa
Rahmal
Washabiki tunasubilia
Hopemwaikuka
Haya tupo
Angelina
Goodupdate
Lydia Emmanuel Magoti
Ngoja tuone
Issa
Saf sana
Issa
Jipange sna
warda
vichwa hatari sana